Sunday, June 17, 2012

Mastaa wa Bongo ni Maharage ya Mbeya




HAKI ya Mungu hii ni aibu kubwa kwa baadhi ya mastaa wa Kibongo wanaopenda kujilegeza kwa wanaume wasiowafahamu na kuondoa utu wao kwa kuthamini fedha, magari na majumba ya kifahari hivyo kusababisha kuitwa ‘Maharage ya Mbeya, maji mara moja!’...

Tabia ya maharage ya Mbeya ni kuiva kwa muda mfupi baada ya kubandikwa jikoni, ndipo kunakofananishwa na tabia ya mastaa hao wa Bongo.


CHANZO CHA HABARI
Kwa mujibu wa chanzo makini, hivi karibuni kuna mtu alijifanya ni mchumba wa mwigizaji Jacqueline Masawe Wolper, Abdalla Mtoro ‘Dallas’ na kuanza kuwatongoza mastaa  mbalimbali kwa njia ya simu ambao nao walijigonga huku wakitaka vitu hivyo vya kifahari ili watoe penzi.
BALAA LA AINA YAKE
Mpashaji wetu huyo alisema kuwa jamaa huyo ambaye ni rafiki wa karibu wa Dallas alifanya mchezo huo ili kuona jinsi mastaa wetu wanavyojiheshimu na kujilinda ndipo akakutana na balaa la aina yake.
Dallas huyo feki alianza kuwatumia ujumbe mfupi (SMS) mastaa mbalimbali kila mmoja kwa muda wake na kuanza kuwashawishi kuweza kumkubali kimapenzi na kuwapa kila kitu ambacho wanakitaka endapo watamkubalia ombi lake la mapenzi.
JAMAA AANZA NA WEMA
Dallas feki alianza kurusha kete yake kwa Wema Isaac Sepetu ‘Tajiri’ ambapo kila alipojaribu kumuweka kwenye mtego mrembo huyo utadhani alijua kwani alichomoa mwanzo mwisho akimweleza kuwa hataki chochote kwani amejikamilisha kila idara hivyo ni bora angeangalia ustarabu mwingine.

SNURA CHUPUCHUPU
Huku kikimwaga majibizano ya SMS za mastaa hao, chanzo hicho kilisema kuwa baada ya Wema kuchomoa, jamaa aliendelea kurusha karata kwa aliyekuwa mwigizaji wa Kundi la Fukuto Arts Promotion waliotamba na mchezo wao wa Jumba la Dhahabu, Snura Mushi ambaye awali alionekana kuingia mkenge lakini aliomba atafutwe baada ya dakika kumi ili afikirie na alipotafutwa tena aliruka kimanga na kusema hayuko tayari.
NI ZAMU YA UWOYA
Chanzo kiliendelea kutiririka kuwa baada ya Dallas feki kugonga mwamba kwa Snura, alijipanga vilivyo akageuzia kibao kwa Irene Uwoya ambaye mwanzoni alionesha kusita kwa kutoamini kama jamaa huyo kweli ni Dallas wa Wolper hivyo akaomba atumiwe meseji ili ajiridhishe kuliko kuongea tu kwenye simu ambapo mazungumzo yalikuwa hivi;

Dallas Feki:  Mimi Dallas na ninaomba chochote nitakachoongea mimi na wewe kiwe siri kati ya mimi na wewe, sitaki Jack (Wolper) afahamu na utaje chochote unachotaka nikufanyie.
Irene Uwoya: Hapana, mimi siwezi kusema kitu ninachokitaka, wewe ndiyo uniambie utanipa nini na uniambie unachotaka kugharamia kwangu.

Dallas Feki:  Ndiyo maana mimi nikakwambia useme utakacho mimi niko tayari.
Irene Uwoya: Kwa upande wangu mimi nina kila kitu na ndiyo maana nikwakwambia wewe unaweza kunifanyia nini, tumia akili yako.

Dallas Feki: Hutamwambia mtu lakini?
Irene Uwoya:  Ndiyo wewe endelea.

Dallas Feki: Tatizo umeshaniambia wewe ni wa gharama, basi nitakupa  gari aina ya BMW X6 na nitakuwekea milioni 16 kwenye akaunti yako. Je, utaweza kuwa na mimi kwa usiku mmoja kwa sababu mimi niko hoi juu yako.
Irene Uwoya: Samahani mimi si wa rahisi kiasi hicho unafikiri siwezi kuwa na X6?

Dallas Feki: Basi bwana naona huna nia na umefikiri kupangiana bei ni busara?
Irene Uwoya: Wewe ndiyo huna nia.

Dallas Feki: Inanishangaza sana kuanza kuuliza ni kiasi gani naweza kukugharamia, sio vizuri hata kidogo kwani mali na pesa hazilinganishwi na utu wako nakutakia kila la kheri.
Irene Uwoya:  Sasa unafikiri X6 ni sare kwa wanawake unaotembea nao, mimi siyo kicheche wa hivyo.

ZAMDA UROJO
Shushushu wetu alitonya kuwa baada ya kumalizana na Uwoya, Dallas feki hakuishia hapo kwani alitupa kamba staa mwingine wa picha za Kibongo, Zamda Salim ambaye walianzia mbali lakini mwisho wa siku, amini usiamini, msanii huyu aliingia kichwa kichwa na kumkubali na kumuomba amtumie namba ya akaunti ya benki ili amtumie mshiko.

Chanzo kilidai kuwa fumba fumbua, Zamda alituma namba ya akaunti fasta huku akimlilia shida zake nyingine ambapo majibizano ya SMS yalikuwa hivi;

Dallas Feki: Naomba unitumie akaunti namba yako ili niweze kukutumia pesa
Zamda:  Akaunti yangu ni 3300....48 ni  KCB (Benki) Dollar account.

Dallas Feki: Nimeipata sasa naomba tukutake Joberg (Johannesburg, Afrika Kusini).
Zamda: Sawa lakini nataka nihame hapa kwaza kwani hapa ninapokaa hakuna ulinzi mpenzi.

Dallas Feki: Sawa nitakulipia lakini ukiri kwanza kuanzia leo mimi  ni mpenzi wako.
Zamda:  Hahahaha ndiyo mpenzi umefurahi?

BADO TUPO MZIGONI
Baadhi ya mastaa wa kike Bongo wamekuwa na tabia hiyo mjini kwani hawana kazi muhimu ya kujishughulisha ili kuweza kujipatia kipata halali matokeo yake kutumiwa hovyo na wanaume kisha kuachwa huku wakidharaulika siku hadi siku.

Hata hivyo, timu yetu bado ipo mzigoni hivyo ripoti kamili inakuja.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...