Sunday, June 17, 2012

KUNA TISHIO LA LULU KUUAWA?



HATIMAYE siri ya kumwekea ulinzi mkali Elizabeth Michael ‘Lulu’ ambaye anakabiliwa na mashitaka ya kifo cha Steven Kanumba imebainika.

Siri hiyo ilitobolewa Jumatatu iliyopita na askari polisi mmoja ambaye hakuwa tayari kuweka hadharani jina, aliyepewa kazi ya kukagua watu wanaoingia kwenye Jengo la Mahakama ya Kuu kwa ajili kusikiliza kesi ya msanii huyo iliyokuwa ikitoa maamuzi ya kujadili umri wa Lulu.

Afande huyo alimtilia shaka mmoja wa waandishi wa habari ambapo ilibidi ampekue sehemu mbalimbali za mwili licha ya kujieleza na kuonesha kitambulisho chake cha kazi.

“Kitambulisho kitu gani bwana, watu wanavitengeneza tu siku hizi, mihuri ya bandia kibao tunapokutilia shaka ni lazima tujiridhishe bwana,” alisema askari huyo huku akiendelea na zoezi la kumkagua paparazi huyo na mwandishi wetu akiwa pembeni.

Yafuatayo ni mazungumzo kati ya mwandishi wetu na askari huyo.
Mwandishi: “Hivi ni kwa nini kitoto kidogo kama hiki mnakiwekea ulinzi wa kutisha kuliko hata muuaji wa kutumia bunduki?”
Askari: “We acha tu, unajua hii kesi ni tofauti kidogo na nyingine, huu ulinzi si kama tunahisi huyu mtoto anaweza kututoroka, hilo halipo. Isipokuwa kuna taarifa kuwa kuna kundi la watu linataka kumdhuru na hata kumuua ndiyo maana tumekuwa tukizidisha ulinzi kila tunapoona kuna haja ya kufanya hivyo.”

Mwandishi: “Kundi hilo ni la akina nani?”
Askari: “Hiyo ni siri ya ndani, lakini sisi tunasema ole wake mtu yeyote atakayenaswa akiwa katika mpango wa kutaka kutekeleza mpango huo au atakayethubutu, yaani naapa atakiona kilichomtoa kanga manyoya.”

Mwandishi: “Mbona alipokwenda chooni alisindikizwa na kundi la askari wa kike na wa kiume, yaani mnahisi hao maadui wanaweza kutekeleza mpango huo hata chooni?”
Askari: “Nimekwambia lengo ni kuimarisha ulinzi, hatuwezi kulegeza ulinzi mahali popote na hivi ninavyokwambia hata ulinzi wa Gereza la Segerea umeongezwa kwa ajili yake, kuna askari wametolewa magereza mbalimbali wameongezwa.”

Mwandishi: “Kwa hiyo mnaamini kundi hilo linalotaka kutekeleza mpango huo lina nguvu kubwa kama nyinyi? Maana mnawatumia askari wenye kofia za chuma, nguo za kuzuia risasi na bunduki aina ya SMG zenye risasi 60, mnaona hazitoshi mnaiwekea ‘magazine’ ya ziada yenye risasi nyingine kama 60 na kuna bunduki zaidi ya 20.”
Askari: “Siku zote unapotaka kupambana na adui yako ni lazima ujikamilishe, huwezi kujua mwenzio amejiandaa vipi, cha msingi sisi tumejiandaa vya kutosha, si unaona huu msafara wa magari matatu na askari zaidi ya 30, tena wenye silaha unazoziona na nyingine huzioni umetoka Segerea kuja hapa kwa ajili ya mtu mmoja.
“Ni gharama kubwa kwa serikali maana kuna askari walitakiwa kwenda likizo lakini wamelipwa kwa ajili ya kusitishiwa likizo zao kwa sababu ya huyu Lulu,” alisema askari huyo.

Akaongeza: “Hali hii ilianza akiwa kituo cha polisi (Oysterbay), kabla Kanumba hajazikwa.
“Hawa watu wakaweka mkakati wa kumpeleka Lulu aliko Kanumba, serikali ikalijua hilo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...