Thursday, May 31, 2012

WEMMA SEPETU ACHUMBIWA TENA: AVISHWA PETE USIKU WA JANA...!!!



Msanii ambaye hajawahi kukaukiwa na matukio yenye kufaa kutengeneza vichwa vya habari katika vyombo vya habari nchini, Wema Abraham Sepetu, kwa mara nyingine ametawala vyombo vya habari baada ya tukio lake la usiku wa jana la kuvishwa pete ya uchumba na msanii wa bendi ya Machozi, anayekwenda kwa jina la Mwinyi.
Tukio hilo ambalo limevuta hisia za wapenzi wa masuala ya udaku na burudani nchini, lilijiri katika ukumbi wa Maisha Club, jijini dar es salaam, usiku wa kuamkia leo, ambapo lilishuhudiwa na mashabiki lukuki wa bendi ya Machozi waliokuwa wamejazana hapo kwa ajili ya burudani ya muziki uliokuwa ukiporomoshwa na bendi hiyo.

Hata hivyo, tofauti na ambavyo imechukuliwa na watu wengi kuwa Wema amepata mchumba mpya na ndio alikuwa akimvisha rasmi pete ya uchumba, ukweli ambao umewekwa wazi ni kuwa, mwanadada huyo alihusika katika tukio hilo kama sehemu ya maandalizi ya filamu yake mpya itakayokwenda kwa jina la Super Star.
Movie hiyo inatarajiwa kuelezea maisha halisi ya msanii huyo ambaye pia aliwika katika medani za ulimbwende, na Mwinyi atashiriki katika filamu hiyo akiigiza nafasi ya mwanamuziki Diamond, ambaye alikuwa mpenzi wa Wema na ambaye alimvisha pete ya uchumba lakini wakamwagana baadae kutokana na mikasa baina yao kuzidi kushamiri.

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI MEI 31



BAADA YA MTAJI, SASA DOGO ASLAY ANAMJENGEA MAMA NYUMBA…… ISIKILIZE SINGLE YAKE MPYA PIA.



Aslay.
Dogo Asley November mwaka jana alimpa mama yake mtaji wa laki tano kwa ajili ya kufanya biashara, leo ametangaza good news nyingine kuhusu kuwasaidia wazazi wake ambao maisha yao yamebadilika kwa kiasi kikubwa baada ya kupewa mitaji ambayo wameweza kuiendeleza vizuri mpaka sasa.
Alichokitangaza leo Dogo Aslay mwenye umri wa miaka 16 ambae muziki pekee ndio unaompa hela, ni kuhusu kuwasaidia wazazi wake kujenga nyumba kwenye kiwanja ambacho kilinunuliwa na mama yake mzazi Gongo la Mboto Dar es salaam miaka kadhaa iliyopita, ametoa zaidi ya laki saba Mwaka huu kuifikisha nyumba mpaka kwenye madirisha na anachotaka ni kumaliza kuijenga ndani ya muda mfupi sana ujao.
Hiki sio kitu cha kawaida, dogo Asley amekua mtoto wa kwanza Tanzania mimi kumsikia akiwa na umri mdogo kama huo lakini katoa kiwango kiwango kikubwa cha pesa kama hicho kumjengea mama yake nyumba.
Aslay amesema “maisha tuliyotokea sisi sio mazuri, nitaendelea na moyo wangu huu huu kwa sababu nikiwaacha wazazi wangu nahisi kama laana itanipata, nataka nikifikisha miaka 17 niwe nimemaliza kumsaidia mama kujenga nyumba, uwezo huo ninao”
Staa huyu ambae single iliyompa nafasi ya kuingia kwenye list ya wakali wa bongo fleva ni naenda kusema kwa mama,  ametoa zawadi nyingine nzuri ya single mpya inaitwa Umbea umbea ambayo pia inahusu ukweli wa maisha ya mama yake ya kunyanyaswa na umbea umbea wa mtaani, kampa shavu Chege.
Isikilize single yake mpya ya Umbea Umbea hapo chini………………….. 

DIAMOND ASEMA ALICHOKIPATA BAADA YA KUPERFORM BIG BROTHER AFRICA!



.









Siku nne baada ya kuperform kwenye shindano la Big Brother Afrika, staa wa muziki Tanzania ambae ndio anaongoza kwa kupiga showz nyingi na zenye hela ndefu, Diamond Platnums amesema baada ya performance yake kuonekana tayari tayari milango mingine ya mafanikio imefunguka.
Amesema “nimepata vitu vingi, imenitengenezea mwanya wa kukubalika sana na karibu media zote za kule nimepata nafasi ya kusain karatasi kwenye baraza la sanaa Afrika kusini ambapo sasa radio zitaanza kucheza nyimbo zangu na nitakua nalipwa wakizipiga, nimepata connection ya kufahamiana na wasanii wakubwa wakubwa wa Afrika ambapo mda sio mrefu nitafanya nao kazi”
Kwenye sentensi nyingine Diamond amesema “Nimewapa album yangu ya kwanza na nyimbo zangu nyingine ambazo nimeshaziachia, nimetafutwa na watu wa media za Nigeria, Namibia na kwingine ambao walitaka niwape kazi zangu, hiyo ni baada ya kuperform kwenye show ya Big Brother japo kabla hawakudhani kama ningeweza kufanya hivyo… na kuna vitu vingine ambavyo nimevipata na sijaruhusiwa bado kuvizungumza ila nitavizungumza na watu wanaweza wasiamini kwamba vimetokana na show yangu BBA”
Bab Tale ambae ni Meneja wa kundi la Tip Top Connection alieongozana na Diamond kwenda Afrika Kusini amesema kwa mara ya kwanza kwenye historia ya shindano la Big Bro, kwenye show ya Diamond mmoja wa mashabiki waliopagawa ndio alipanda kwenye stage na kwenda kucheza kitu ambacho huwa hakiruhusiwi, ni masharti ambayo huwa wanapewamashabiki wote wanaokwenda kutazama show, hivyo baada ya huyo mmoja kuvunja sheria, alitolewa nje.
Tale amesema toka walipotoka bongo walipitia Nairobi na hakuna mtu aliewashangaa, yani mpaka Tale akawa anajiuliza moyoni mbona watu hata hawashtuki, walipofika pia South Afrika hakuna aliewashangaa hata walipokua wanaanza mazoezi watu waliowapokea walikua wanamchukulia poa Diamond lakini alipoanza mazoezi wakajua jamaa mkali, kwa maelezo mengine zaidi msikilize Bab Tale hapo chini…………

MAHABA: WANAUME WANAOONGOZA KWA KUVUNJA NDOA ZA WATU



NDUGU zangu, katika maisha ya sasa kuna watu flani ambao ukiona wana ukaribu uliopitiliza kwa mke wako, jua kuna jambo nyuma ya pazia na ukishangaashangaa unaweza kujikuta unamegewa penzi lako hivihivi.
Hiki nitakachokielezea leo nimekifanyia uchunguzi wa muda mrefu na kwa wale waliokumbana na hali halisi ya mambo, watakubaliana nami kwa asilimia zote. Juzi nilipata bahati ya kusuluhisha ugomvi wa rafiki yangu ambaye yeye na mkewe ni wafanyabiashara.
Chanzo cha ugomvi wao ni daktari mmoja ambaye inaonekana kwa muda mrefu amekuwa ‘akiitafuna’ ndoa yao na siku hiyo ndiyo ule msemo wa za mwizi arobaini ulipotimia. Rafiki yangu huyo alinasa sms kutoka kwa dokta huyo akitaka wakutane na mkewe siku hiyo.
Bahati ni kwamba, mwanaume huyo alikuwa akimpenda sana mke wake na hata nilipomshauri amsamehe waanze ukurasa mpya, alinielewa.
Lakini wakati hilo likitokea, jana yake nilisoma habari ya mke wa mtu aliyefumaniwa na kijana mmoja ambaye ni muuza genge mtaani kwao. Aibu ilioje kwa mwanamke huyo! Hivi inakuwaje mpaka mke wa mtu ambaye mume wake anahangaika juani kutafuta noti kisha mkewe huku nyuma anatoa penzi kwa muuza genge kirahisi? Hii inauma sana!
Matukio hayo mawili yalinifanya nifikie hatua ya kuandika makala haya juu ya watu wanaongoza kwa kusambaratisha ndoa za watu.
Muuza genge
Kuna tabia ambayo baadhi ya wanawake walio katika ndoa wanayo ya kubana matumizi yao ya kila siku kwa lengo la kuweka fedha za kufanyia mambo mengine baadaye.
Katika mazingira hayo wapo wanaojiweka karibu sana na watu hao wakiamini watapewa vitu vya bure kama vile nyanya, vitunguu nk. Wanawake wa sampuli hii wakikutana na wauza genge viwembe hawawezi kupona na ndiyo maana mwanaume anashauriwa kuwa makini sana na wauza magenge.
Mwalimu
Hapa nazungumzia zaidi walimu wa vyuoni. Baadhi yao wamekuwa wakiwarubuni wanawake kwa kuwaahidi kuwafaulisha kwenye mitihani na wamekuwa wakiwatishia kuwafelisha endapo watawachomolea. Hilo limekuwa likiwafanya baadhi ya wanawake wasio na msimamo kuwa tayari kwa lolote ili mradi wafaulu.
Dereva bajaji, teksi
Nani asiyejua kuwa baadhi yao wanaongoza kwa ukware? Kwa kifupi hawa ni miongoni mwa watu ambao mwanaume hatakiwi kukubali ukaribu uliopitiliza kwa wake zao kwani historia inaonesha wengi wao wamekuwa wepesi wa kuomba penzi hasa mazoea yanapovuka mipaka.
Muuza duka
Mama mmoja ambaye mume wake anafanya biashara za kusafiri mikoani alinaswa na mpangaji ambaye kwenye nyumba anayoishi mwanaume huyo ana duka. Baada ya tukio hilo ilibainika mama huyo alikuwa na tabia ya kuchukua vitu dukani hapo na siku hiyo alipotakiwa kulipa alimwambia kimasihara kuwa, yeye hana fedha kama vipi wamalizane kwa njia nyingine.
Kama mwanamke huyu alivyosema, wapo wake za watu ambao wamekuwa wakijirahisi sana kwa wauza duka wakijua itakuwa rahisi kwao kuambulia vitu vidogodogo na fedha. Kwa maana hiyo mkeo si wa kumruhusu kuwa na uhusiano wa karibu sana na wauza duka.
Mganga wa kienyeji
Wapo waganga wa kienyeji ambao ni wasanii tu. Katika hawa wanaodaiwa kuwa wasumbufu kwa wake za watu ni wale wanaojidai kutibu magonjwa ya kinamama.

JESTINA GEORGE ON AFRICAN FASHION & DESIGNS


Jestina George is a fashionista, blogger, Presenter and a model based in London, from Tanzania the land of Kilimanjaro. AILTV caught up with her at the the launch of READY TO WARE by Anna Luks. Jestina is speaking,  expressing her concerns about African fashion and designs.

SEREMALA WA MAGOMENI DAR APIGWA NA WANAJESHI KWA SIKU TATU



Fundi Haule akiwa amelala bila kujitambua baada ya kupigwa na kuburuzwa kama mzigo.

…Akiwa anachuruzika damu na kugumia kwa maumivu.

Wananchi waliofika eneo la tukio.

Haule (katikati) akipelekwa hospitali baada ya ndugu zake kujitokeza.

KIJANA mmoja aliyetambulika kwa jina moja la Haule ambaye ni fundi seremala amepata kipigo cha nusu ya kufa kutoka kwa mteja wake aliyedaiwa ni mwanajeshi na ambaye aliongozana na wanajeshi wenzake wawili kumshambulia.
Tukio hilo la aina yake lililosababisha wananchi kibao kujitokeza sehemu hiyo, limetokea maeneo ya Magomeni-Morocco jijini Dar es Salaam ikiwa ni siku ya tatu kupokea dozi hiyo iliyomuacha akiwa mahututi huku damu zikimtoka baada ya watu watatu waliojitambulisha kuwa ni wanajeshi kumshushia kipigo kutokana na mmoja wao kumdai kitanda ambacho alishamlipa laki tatu ili amtengenezee.
Baada ya kumshushia kipigo fundi huyo, wananchi walijitokeza ambapo walifanikiwa kuwakamata wanajeshi wawili na kuwapeleka katika kituo cha polisi Magomeni huku mmoja akifanikiwa kuwatoroka, jambo ambalo lilisababisha machafuko ya muda mrefu ambapo polisi walichelewa kufika eneo la tukio.

MASTAA WASHINDANA KUANIKA MAPAJA YAO





Aunt Ezekiel.

Mayasa Mrisho ‘Maya’.

Jennifer Kyaka ‘Odama’.
SURA za mauzo kwenye anga la Bongo Movies, Jennifer Kyaka ‘Odama’, Aunt Ezekiel na Mayasa Mrisho ‘Maya’ walifunikana kwa kuvaa nguo zenye kuacha mapaja yao nje hali iliyozua ‘muwashawasha’ kwa wanaume wenye tamaa za mahaba.
Ishu hiyo ilichukua nafasi juzikati kwenye Ukumbi wa Nyumbani Lounge, jijini Dar ambapo mastaa hao walialikwa kusherehekea uzinduzi wa bidhaa mpya ya kinywaji.
“Mh! Jamani hawa wametufanyia makusudi kushindana kuvaa viguo vifupi, hawajui kuwa wanatupa wakati mgumu?” alisikika akihoji mdau mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Dick.

SAJUKI AFANYIWA UPASUAJI



Sadick Juma Kilowoko ‘Sajuki’ hospitalini.
HATIMAYE, staa wa filamu za Bongo, Sadick Juma Kilowoko ‘Sajuki’ amefanyiwa upasuaji wa tumbo kufuatia matatizo yanayomsumbua...
Akizungumza Jumatatu iliyopita kwa njia ya simu tokea Mumbai, nchini India alikolazwa mumewe, mke wa Sajuki, Wastara Juma alisema madaktari wamefanikisha upasuaji huo, lakini hali ya mgonjwa huyo ikawa mbaya ghafla.
Aliongeza kuwa kufuatia hali hiyo, maombi yanahitaji kwa Watanzania ili mumewe arejee katika hali inayotazamiwa na madaktari.
Hata hivyo, Jumanne iliyopita, Wastara alizungumza tena na mwandishi wetu ambapo alisema Mungu ni mkubwa, hali ya mumewe anatengemaa na ameanza kunyanyuka baada ya upasuaji huo.
“Hali imekuwa nzuri, sasa ananyanyuka si kama alivyotoka kwenye chumba cha upasuaji, lakini Watanzania wazidi kumwombea,” alisema mwanadada huyo.
Katika hali nyingine isiyokuwa ya kawaida, Wastara alisema akiwa hospitalini hapo, madaktari wameidaka kamera yake na kuiweka mapokezi wakimtuhumu kuitumia vibaya.
Walimwambia kuwa ni kosa kwa mtu kutumia kamera yake kupiga picha bila ridhaa ya utawala. Hata hivyo, msanii huyo alisema atarudishiwa kifaa chake hicho cha kuchukulia picha kwani alitoa barua kutoka Shirikisho la Filamu Tanzania ‘TAFF’ inayoonesha yeye ni msanii wa muvi nchini.
Sajuki, yuko nchini humo akitibiwa matatizo ya vimbe tumboni. Aliondoka nchini katikati ya Mei, 2012 kwa ajili ya kufuata matibabu.

LULU AWATESA ASKARI




Lulu akiwa mahakamani.

...Akiwa chini ya ulinzi mkali ndani ya mahakama.

...Akishushwa kwenye gari.

Askari waliokuwa kwenye gari wakiwa tayari kumlinda msanii huyo.

Maaskari wakiwa na silaha zao tayari kwa lolote.
IMEBAINIKA kuwa staa wa picha za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ anawapa wakati mgumu askari magereza na polisi kufuatia ulinzi mzito wanaolazimika kumpatia wakati wa kumpeleka mahakamani na kumrejesha mahabusu kwenye Gereza la Segerea, Dar es Salaam...
Baada ya wiki kadhaa mambo kutulia na ulinzi kuwa wa kawaida tofauti na siku ya kwanza alipofikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Jumatatu wiki hii hali hiyo ilijirudia ambapo Lulu ambaye anakabiliwa na kesi ya kifo cha Steven Kanumba alifikishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam akiwa na ulinzi wa kutisha.
HOT POT ilimshuhudia Lulu akishushwa mahakamani hapo akiwa mtuhumiwa pekee kwenye basi huku akisindikizwa na askari magereza wanawake zaidi ya kumi.
Mbali na askari magereza wanawake, kulikuwa na difenda la magereza lenye king’ora lililokuwa limejaa askari magereza wanaume na polisi wa kawaida.
ULINZI MAHAKAMANI
Mara baada ya ‘Kalulu Kadogo’ kufikishwa mahakamani hapo walipokezana na polisi wa mahakamani na katika kufumba na kufumbua, kila kona kulikuwa na askari waliokuwa wameimarisha ulinzi nje na ndani ya eneo hilo.
Maafande hao walishuhudiwa wakiwa wamevaa majaketi yasiyopenya risasi (bullet proof), kofia za chuma huku wakiwa na ‘mabunduki’ aina ya SMG zilizokuwa zimejaa risasi na mikanda ya risasi za ziada.
Wakati baadhi wakitanda ndani ya mahakama wakiwa wamemzunguka Lulu, wengine walizagaa nje huku wakizuia watu kukatizakatiza ovyo.
WAOMBA MAMBO YAISHE
HOT POT ilizungumza na baadhi ya askari hao wa kike ambao walionekana kutamani kesi hiyo iendeshwe haraka ili mambo yaishe kutokana na mshikemshike wanaokutana nao wakati wa kumpeleka Lulu mahakamani na kumrejesha gerezani.
Kuna baadhi waliokwenda mbali wakidai wanatamani hata kuhama vituo vyao vya kazi kutokana na mikikimikiki wanayokutana nayo wanapotakiwa kumpeleka Lulu mahakamani.
Ilidaiwa kuwa inapofika siku ya kumpeleka Lulu mahakamani, hulazimika kusitisha udhuru wowote kama kuwa wagonjwa hivyo kuzishangaza familia zao kwani wanapoulizwa kulikoni wanasema ni siku ya staa huyo na kila askari anakuwa ‘stendibai’.
Kwa muda wa saa mbili mahakamani hapo huku mawakili wakibishana juu ya umri wa Lulu, ratiba zote zilisitishwa kwani shughuli ilikuwa ni hiyo tu.
‘AMA KWELI ANAWATESA ASKARI’
“Ama kweli Lulu anawatesa hawa askari, kila mmoja yuko ‘bize’ na suala la ulinzi wake,” alisikika dada mmoja aliyefika mahakamani hapo kufuatilia kesi hiyo.
KESI YAPIGWA KALENDA
Baada ya mawakili hao kushindwa kufikia muafaka wa umri kama ni miaka 17 au 18, kesi hiyo ilipigwa kalenda hadi Juni 11, mwaka huu ndipo utata wa umri wa Lulu utakapopatiwa ufumbuzi ili kuruhusu kesi hiyo ianze kusikilizwa.
TUMEFIKAJE HAPA?
Lulu ni mshukiwa wa kwanza katika kesi ya kifo cha aliyekuwa mpenzi wake na staa mkubwa wa filamu za Kibongo, Kanumba aliyefariki dunia Aprili 7, mwaka huu nyumbani kwake maeneo ya Sinza Vatican City, Dar.

Wednesday, May 30, 2012

WEMA, JOKATE NUSURA WAZICHAPE





Wema Sepetu.

Jokate Mwegelo.

Naseeb Abdul ‘Diamond’.
MASTAA wa kike wanaotambiana Bongo, Wema Sepetu na Jokate Mwegelo, ilibaki kidogo wazichape kavukavu kisa kikiwa kilekile, msanii anayetingisha katika Bongo Fleva, Naseeb Abdul ‘Diamond’.
Chanzo chetu makini kimenyetisha kwamba mtiti huo ulitokea Ijumaa Mei 25, mwaka huu katika Ukumbi wa Blue Pearl, Ubungo, Dar ambapo kulikuwa na Shindano la Miss IFM, 2012.
CHANZO KINADADAVUA
Katika ‘event’ hiyo, Wema alikuwa mmoja wa majaji waliochagua washindi wakati Jokate alifika kama mdau wa urembo huku uwepo wa Diamond ukiwa kwa ajili ya kupiga shoo.
“Wema alikuwa mmoja wa majaji, Jokate alikwenda kama shabiki tu, lakini mambo yalianza kuharibika baada ya mshindi kutangazwa ambapo Jokate hakuridhishwa na matokeo.
“Hata hivyo, watu walisema ni chuki zilizosababishwa na wivu wa kimapenzi kwa Diamond,” chanzo kilieleza.
JOKATE ALIANZA HIVI
Habari zinasema kwamba, Jokate aliamua kupita mbele ya meza ya majaji na kumuuliza Wema kama yeye aliridhika na matokeo yale.
“Ilikuwa balaa, Jokate alikwenda kwenye meza ya akina Wema (majaji), akaanza kumuuliza, yaani huyu ndiyo mshindi mliyetuchagulia? Miss gani anakuwa hivyo?” kilisema chanzo na kuongeza:
“Kifupi alikuwa akitoa kejeli kwa majaji hasa Wema kwa vile aliwahi kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya dunia.”
WEMA AKAMALIZA
Baada ya chokochoko za Jokate ambaye inasemekana alikuwa ‘amechangamka’ kidogo, Wema alijibu mashambulizi kwa staili ya aina yake, alikaa kimya akiendelea na shughuli nyingine.
“Ukimya wa Wema ukasababisha Jokate azomewe kwa sauti kubwa na mashabiki huku wakimsonya. Kiukweli bila ushabiki, Wema alionesha ukomavu siku ile.
“Kama naye angepandisha hasira, ilibaki kidogo sana wakung’utane, maana Jokate alionekana dhahiri kutaka ugomvi lakini mashabiki wakaununua kwa kumzomea. Aliabika sana,” kiliendelea kupasha chanzo hicho.
DIAMOND AAMSHA SOO UPYA
Wakati Diamond akiwa jukwaani ‘akipafomu’ wimbo wa Nimpende Nani? ikawa kama ameamsha ‘muziki’ upya kabisa kwa upande wa Jokate.
“Diamond alipouliza nimpende nani? Watu wakawa wanapiga kelele wakisema, Wemaaaa, lilipotamkwa jina la Jokate, ilifuatiwa na zomeazomea, hali hiyo ilizidi kumpa Jokate wakati mgumu.”
Habari zinadai, hali ilizidi kutibuka zaidi baada ya mashabiki kumzonga Wema wakimtaka kupiga naye picha huku wakimtupia vijembe vya wazi Jokate.
JOKATE APOTEA GHAFLA
Kutokana na hali hiyo, Jokate alishindwa kuvumilia kashikashi za mashabiki waliokuwa upande wa Wema, hivyo akatoweka ukumbini humo.
Chanzo kikaendelea kufafanua kuwa kuna wakati alitafutwa kwa ajili ya kupiga picha ya pamoja na washindi waliotinga Tatu Bora wakiongozwa na Miss IFM 2012, Fina Revocatus aliyeshinda lakini bila mafanikio.
WEMA ANASEMAJE?
Baada ya madai hayo, mapaparazi wetu walianza kazi ya kumsaka Wema ili aeleze anachokijua kuhusu habari hiyo ambapo walifanikiwa kumpata siku ya pili ya tukio, Mei 26 mwaka huu na kutoa ushirikiano wa kutosha.
Akizungumza kwa njia ya simu na paparazi wetu, Wema alikiri kutokea kwa tafrani hiyo akisema ameiona nguvu ya jamii katika kusimamia ukweli.
Huyu hapa mwenyewe anafunguka: “Malipo ni hapa hapa duniani. Namshukuru Mungu, aibu haikuja upande wangu, nimeamini mashabiki wengi walisimama na mimi na ukweli ulijulikana.
“Siku zote penye ukweli, uongo hujitenga. Kila mtu ameamini kuwa kuachana kwangu na Diamond sikuwa na makosa. Sikunyanyua mdomo wangu kusema chochote, mashabiki ndiyo wamekuwa mabalozi wangu. Niseme nini tena?”
JOKATE NAYE?
Jitihada za kumpata Jokate ziligonga mwamba baada ya simu yake ya mkononi kutokuwa hewani kila alipopigiwa.
Hata hivyo, ‘polisi’ bado wapo mzigoni wakiendelea kumsaka atakapopatikana mbivu na mbichi zitawekwa peupe.

KUMBUKUMBU MUHIMU
Wema na Jokate walichuana vikali katika Shindano la Miss Tanzania mwaka 2006 ambapo Wema alitwaa taji na Jokate kuchukua nafasi ya pili.
Wote wawili, nje ya fani ya urembo, wamejaribu kwenye ulingo wa filamu. Hakuna ubishi kuwa Wema ndiye aliyefanikiwa zaidi kuliteka soko la sinema za Bongo huku Jokate akipiga hatua moja zaidi kwenye mitindo.
TUMEFIKAJE HAPA?
Awali, Wema aliwahi kuwa mpenzi wa Diamond na kumwagana kabla ya kurudiana na kuendelea na penzi lao.
Baadaye wawili hao wakamwagana tena huku Wema akitoa madai mazito kuwa shogaye Jokate alikuwa akitoka na shemeji yake, Jokate alikanusha kwa nguvu zote.
Kukiwa bado kuna wingu la sintofahamu, penzi la Jokate na Diamond likawa peupe kabla ya wiki chache zilizopita kudaiwa kwamba limevunjika.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...