Thursday, June 21, 2012

MAMA: UWOYA KALA RAMBIRAMBI ZA KANUMBA




KUNA habari kwamba mama wa marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa, ‘picha haziendi’ na mwigizaji wa filamu za Kibongo, Irene Uwoya kutokana na mama huyo kudai fedha za rambirambi kwa Uwoya alizodai amezila.
Hivi karibuni Uwoya na wenzake Patchou Mwamba na Juma Chikoka ‘Chopa’ walikuwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kumalizia msiba wa swahiba wao huyo.

Akizungumza hivi karibuni, Chopa aliyekuwa miongoni mwa walikuwa nchini humo, alisema kuwa baada ya kurejea nchini, mama Kanumba aliwataka waende nyumbani kwake na fedha za rambirambi walizopewa kama pole wakiwa Kongo, jambo lililoshangaza sana.
“Sisi tulikwenda Kongo kwa heshima ya marehemu Kanumba na pia kuendeleza uhusiano mzuri aliokuwa ameanza kuutengeneza ndiyo maana wengine wamejilipia nauli. Kutudai rambirambi kumetushangaza sana, anategemea hizo fedha zitatoka wapi?” alisema Chopa kwa mtindo wa kuhoji.
Kwa upande wa Uwoya, alipoulizwa kuhusu ishu hiyo, alikiri kuwa ni kweli amesikia kuwa mama Kanumba anadai rambirambi za msiba wa mwanaye kwa wasanii waliokuwa nchini Kongo akiwemo yeye na kueleza masikitiko yake.




“Sasa mama Kanumba anategemea hizo fedha tunazitoa wapi? Hajui jinsi tulivyopata shida ya usafiri wa kwenda na kurudi, wengine tumelazimika kujigharamia wenyewe nauli, hii yote ikiwa ni kumuenzi mwenzetu, sasa yeye anadai fedha za kutoka wapi?” alihoji Uwoya.
Baada ya kusikia kutoka upande mmoja wa wasanii waliokwenda Kongo, Risasi Mchanganyiko lilitenda haki kwa kutafuta mzani wa madai hayo kutoka upande wa pili, likamvutia waya Mama Kanumba ambaye alitoa ushirikiano.

Mama Kanumba alisema, ameshangazwa sana kusikia kuwa Uwoya na wenzake wamesafiri kwenda Kongo kwa ajili ya kumalizia msiba wa mwanaye bila kumpa taarifa akahoji; Nani amewapa ruksa ya kufanya hivyo?
Mama wa marehemu Steven Kanumba.

“Nimesikia wamekwenda Kongo kumalizia msiba wa mwanangu lakini mpaka sasa sijajua mwanafamilia gani aliyewapa ruksa ya wao kwenda huko. Pia sijapewa chochote walichorudi nacho kutoka huko.

“Uwoya na wenzake walete pesa za rambirambi za mwanangu walizopewa Kongo vinginevyo hatutaelewana,” alisema Mama Kanumba.

Marehemu Steven Kanumba.
UHUSIANO WA UWOYA, PATCHOU, CHOPA NA KANUMBA
Kwa namna moja au nyingine, Uwoya na Patchou Mwamba walisaidiwa sana kuingia katika sanaa ya uigizaji na marehemu Kanumba.

Uwoya alitokea kwenye tasnia ya urembo na Patchou akiwa ni mwanamuziki wa Bendi ya FM Academia, kazi anayoifanya hadi sasa.
Kwa upande wa Chopa, alianza kujuana na Kanumba tangu wakiwa pamoja katika Kundi la Kaole Sanaa. Ukaribu wao na marehemu ndiyo uliowafanya wasafiri hadi nchini Kongo kumalizia msiba wa swahiba wao huyo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...