Tuesday, April 10, 2012

YALIYOJIRI LEO LIVE KUTOKA LEADERS CLUB KWENYE MAZISHI YA STEVEN KANUMBA

 
































Matayarisho ya kuuombea mwili wa Kanumba yakifanyika.

Jeneza la mwili wa Kanumba likiwasili  Viwanja vya Leaders.

Sehemu ya umati uliofika hapo.





Baadhi tu ya watu waliodondoka na kupoteza fahamu.

Mmoja wa wanakamati ya mazishi, Mkurugenzi wa Global Publishers, Eric Shigongo (kulia) akimsaidia mama mzazi wa Kanumba (katikati) kwenda kwenye kiti chake.

Makamu wa Rais, Gharib Bilal (kushoto) na Waziri wa Habari na Utamaduni Emmanuel Nchimbi wakiwa msibani.

Msanii wa maigizo, Steven Nyerere anayecheka (kulia) akiwa na Wence Mtuhi (mwenye miwani) ambaye alitoa magari yake kuchukua mwili wa Kanumba.

Baadhi ya wasanii waliofika hapo.

Waombolezaji wakisubiri msafara wa Bilal upite.

Msanii wa filamu Mahsen ‘Dk. Cheni’ akiteta jambo na Wence Mtuhi.





Mmoja wa waombolezaji akisaidiwa na watu wa Msalaba Mwekundu baada ya kuzirai.

Msanii wa filamu, Blandina Chagula akilia kwa huzuni

Mwimbaji wa muziki wa Injili kutoka Kenya, Solomon Mukubwa (kulia) naye alikuwepo.

Mcheza sinema, Wema Sepetu, akisaidiwa na msanii mwenzake, Emannuel Miyamba.

Msanii Irene Uwoya akihudumiwa na wafanyakazi wa Msalaba Mwekundu.

Msanii Rachel Haule akiwa na majonzi.

Waombolezaji wakisukumana kuingia makaburini.




Wema sepetu muigizaji na aliekuwa ex-girlfriend wa hayati Steven Kanumba alizimia baada kuona jeneza la Kanumba likielekea makaburini leo hii mchana,kinondoni Dar.

UMATI mkubwa ulijitokeza leo asubuhi katika Viwanja vya Leaders vilivyopo Kinondoni jijini Dar es Salaam kuuaga mwili wa aliyekuwa msanii wa filamu nchini hayati Steven Kanumba.

Watu wengi, hususan kina mama waliangua vilio mwili huo ulipopita mbele yao na wengine kudondoka na kupoteza fahamu, hali iliyosababisha watu wa huduma ya kwanza kuwa katika kazi kubwa.



No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...