Sunday, April 15, 2012

MATOKEO YA KILLI MUSIC AWARDS 2012



Isha Mashauzi akiwa na tuzo ya Wimbo Bora wa taarab.

Queen Darin akiwashukuru mashabiki waliompigia kura.

Ally Kiba akiwashukuru mashabiki waliompigia kura.

Kiongozi wa African Stars, Luiza Mbutu (katikati), akiwa na tuzo ya Wimbo Bora wa Kiswahili.

Diamond na Ommy Dimpozi wakikamua.

Msanii wa filamu, Shilole akipozi mbele ya kamera.

Diamond akipozi kupiga picha na mama yake.

Mmoja wa akina dada walioudhuria hafla hiyo akihojiwa na mwandishi wa habari.

Diamond akipozi na shabiki wake.

Ally Kiba akielekezwa sehemu ya kukaa.

Wanamitindo Asia Irdaous (kushoto) na Ally Rehmtullah.

Salma Jabu 'Nisha' akiwa na Flora Mvungi. 

Shabiki wa muziki akifuatilia utoaji tuzo huo.

H. Baba na mchumba wake Flora Mvungi.




Msanii aliyejinyakulia tuzo tatu za Kili, Naseeb Abdul 'Diamond' (wa tatu kulia) akiwa katika pozi na vijana wake pamoja na tuzo. Diamond alishinda Tuzo ya Mtumbuizaji bora wa kiume, Mtunzi bora wa mwaka na Video bora ya muziki ya mwaka.

Diamond akiwashukuru mashabiki wake.

Msanii Ommy Dimpoz  aliyejishindia tuzo mbili akipokea tuzo ya Wimbo bora wa kushirikiana alioimba na Ali Kiba. Pia alitwaa tuzo ya Msanii bora anayechipukia.

Babu Tele akinyanyua juu tuzo kwa niaba ya Suma Lee aliyepata tuzo mbili katika hafla hiyo. Tuzo hizo ni Wimbo bora wa mwaka na Wimbo bora wa Afro Pop.

Roma Mkatoliki akiwa na mojawapo ya tuzo zake. Msanii huyo alijipatia tuzo mbili ya Msanii bora wa Hip Hop na Wimbo bora wa Hip Hop.

Kiongozi wa Bendi ya Twanga Pepeta, Luiza Mbutu akiwa na tuzo ya Wimbo bora wa Kiswahili (Bendi).

Msanii Ali Kiba akiwa na tuzo yake ya Wimbo bora wa Zouk/Rhumba.

Isha Mashauzi akifurahia tuzo yake ya Wimbo bora wa Taarab.

AT akiwa na tuzo yake ya Wimbo bora wenye vionjo vya kiasili.

Wasanii wa Kundi la Warrior from the East wakiwa na tuzo yao ya Wimbo bora wa Reggae.

Mwakilishi wa Msanii Jaguar akiwa na tuzo ya Wimbo bora wa Afrika Mashariki.

Malkia wa Mipasho nchini, Khadija Kopa akishukuru kwa tuzo yake aliyoipata ya Mtumbuizaji bora wa kike.

Mtayarishaji wa muziki, Maneck akipokea tuzo yake ya Mtayarishaji (Producer) bora wa nyimbo wa mwaka.

Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo ulijaa shangwe na vifijo wakati wanamuziki wa Bongo walipokuwa wakitunukiwa zawadi za umahiri wa sanaa hiyo zijulikanazo kama KILI MUSIC AWARDS 2012.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...