Friday, April 27, 2012

EXCLUSIVE: MLINZI KWENYE JENGO ILIPOFANYIKA VIDEO YA NAI NAI AACHA KAZI BAADA YA VIDEO HIYO KUMLETEA MATATIZO KAZINI.


.
Aliyekua mlinzi wa zamu kwenye jengo la Amani lililoko mtaa wa Ohio Dar es salaam, jengo ambalo ilifanyika video ya NAI NAI ya Ommy Dimpoz na Ally Kiba, Mganga Msabila aliyekua ameajiriwa na Ultimate Security ameamua kuacha kazi hiyo ya ulinzi baada ya video hiyo kumletea matatizo kazini.
Mganga amesema “tumepata mamtatizo wakati meneja mwenyewe wa jengo aliruhusu hiyo video ifanyike japo alionya kwamba tuhakikishe kina Ommy Dimpoz hawachafui eneo wala kuharibu chochote, siku ya tukio walifanya video yao na mpaka tunakabidhi lindo walikua wanaendelea”
Kwenye sentensi nyingine, Mganga amesema “baada ya siku mbili tuliitwa kwenye makao makuu ya kampuni yetu kule Ultimate Security tukaenda kuandikisha maelezo jinsi ilivyokua, baada ya pale tulijua ishu imekwisha na mwaka 2011 ukamalizika manake video ilifanyika november, lakini tukashangaa tukaja kuitwa tena February 2012 tukaitwa tena makao makuu kutoa maelezo sisi tumeruhusuje ile video kufanyika pale, ishu iliibuka upya baada ya wenye jengo kuona ile video inapigwa sana kwenye TV na pia wanasema ina Ommy Dimpoz wamecheza mpaka ndani ya jengo lakini mimi mpaka nakabidhi lindo kina Ommy Dimpoz hawakua wameingia ndani”
Msabila ambae ni baba wa watoto wanne ambao wanamtegemea peke yake huku mkewe akiwa ni mama wa nyumbani, ameamplfy zaidi kwamba “wenye jengo walikasirika baada ya kuona hiyo video wakatuma tena Taarifa kula makao makuu ya kampuni yetu na walituma na cd nzima ya ile video na wakawa wanahoji kwa nini hawa walinzi waliokuepo zamu siku hiyo hawajafanyiwa kazi? kitu ambacho kilitupa adhabu ya kukatwa mshahara kwa muda wa miezi sita au mwaka kwa sababu wanasema wanatuchunguza, kwa hiyo nikaona haina haja ya kuendelea na kampuni yao ngoja niondoke tu, kosa sio langu limekuja kuwa langu lakini sisi ndio tunashushiwa hayo mambo, nimeona nisije nikaangamiza wengi kwa kosa hilo dogo ngoja nijiengue na mwenzangu nae amejiengua”
Mganga Msabila ambae alipita jeshini kabla ya kuanza kufanya kazi ya ulinzi chini ya kampuni binafsi, kwa sasa amerudi kijijini kwao Sengerema wilayani Chanika mkoani Mwanza ambako ndio familia yake ilipo, anasubiri kama itatokea tena akapata nafasi ya kazi ya ulinzi popote, Ommy Dimpoz ameahidi kuzungumza na millardayo.com soon, so endelea kuchek.
.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...