Friday, April 20, 2012

ALICHOKUTANA NACHO AY KWENYE SHOW SUDAN KUSINI.



Hii ilikua post ya AY kwenye fB wakati akiwa Sudan.
Baada ya kurudi Bongo akitokea Sudan Kusini alikokwenda kupiga show kwa mara ya kwanza japo wamekua wakimwalika toka zamani, AY ameamplfy kwamba hakua na hofu yoyote kwenda kwenye hiyo nchi ambayo iko vitani.
Amesema “ulinzi ulikua mzuri kwangu nilikua nalindwa karibu na askari nane ambao wote wana AK 47 poamoja na convoy, nilikua nalindwa mimi pamoja na watu wangu wanne nilioenda nao, tulikua tunalindwa mpaka usiku tunapokwenda kulala”
Baada ya kufanya show ya kwanza Ay amesema jamaa waliikubali sana ikabidi wamwalike kwenye show nyingine ya pili ambayo ingefanyika kesho yake lakini ikashindikana baada ya kupokea simu kutoka jeshini kwamba vita imeanza hivyo kila kitu kikasimama, simu zikakatwa network, umeme hakuna, ndege za kivita zikasikika huku wanajeshi wakipita kwenda vitani.
Ay alipiga show alhamisi iliyopita huko Juba Sudan Kusini ambapo baada ya show ya pili kufutwa, jamaa wakamkabidhi mkwanja wake na kesho yake asubuhi wakamsindikiza mpaka Airport lakini wamemualika tena kwenye show nyingine mbili ikiwemo moja miezi minne ijayo katika sherehe za Uhuru ambazo zimeandaliwa na serikali.
Kwa furaha AY amesema “moja kati ya vitu nilivyokutana navyo vikamshangaza ni pale ambapo nilikua nakula usiku likapita kundi la wanajeshi alafu wakasema wewe ni AY wewe tunakujua wewe, hata alienipeleka Sudan alishangaa… wale wanajeshi wakaniuluza tena wapi mwanaFaa wakimaanisha Mwana FA, nikasema ahhh kumbe hata mgosi nae wanamtambua………. kingine ambacho kimenishangaza zaidi ni kwamba hela yao ni kubwa kuliko ya nchi yeyote Afrika Mashariki”

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...