Saturday, April 14, 2012

ALICHOKISEMA MBUNGE HALIMA MDEE KUHUSU MWIGIZAJI LULU.


Halima Mdee
Mbunge wa Kawe kupitia CHADEMA Halima Mdee amekiri kwamba kuna baadhi ya watu waliopinga au kutofautiana nae baada yakutangaza uamuzi wa kumsadia mwigizaji LULU ambae sasa hivi yuko gerezani SEGEREA kwa tuhuma za mauaji ya mwigizaji STEVEN KANUMBA.
Amesema “kitu ambacho nimefarijika ni kwamba kama kuna watu 50 wanaotoa comments basi arobaini zitakua zinasupport, na 10 zitaponda na ni kitu ambacho ni cha kawaida sana kwa sababu kila mtu anatafsiri kivyake”
Halima amesema “kweli nimeguswa sana na msiba wa Kanumba, kilichonifanya kwenda kumuona Lulu akiwa chini ya ulinzi wa polisi na nikakutana pia na mama yake nikajua kwamba inawezekana kabisa kuna upande wa pili wa hadithi ambao unahitaji sauti yake kusikika kwa sababu wengi katika hatua za mwanzo tumemuhukumu sana ikizingatiwa kwamba ni mtoto mdogo, nikashawishika tu kwenda kutaka kujua kwa sababu na mimi nilikua simjui, namsoma tu kwenye magazeti”
Kwa kuamplfy zaidi, Mdee amesema “siwezi kusema kwamba hajafanya kosa, hapana kwa sababu hakuna mtu aliekuepo zaidi ya hao wawili na pia nikagundua kwamba ni mtu ambae ana uhitaji sasa hivi hasa ukizingatia umri wake, kumbe pamoja na utoto wake familia yake ndio ilikua inamtegemea yeye, tunajua kesi kama hizi ambazo zina presha kubwa sana ya umma, tunaweza kujikuta kwamba ule ukweli halisi ambao ungeweza ukajulikana unaweza kuzuiwa kujulikana kwa sababu ya presha ya Umma”
“Kimsingi sitaki kulizungumza sana hili ili nisiingilie maswala yanayoendelea mahakamani lakini tulivyoenda bahati nzuri walikuwepo hata baadhi ya maofisa wa polisi ambao walisema kabisa kwamba jana yake Lulu alipelekwa hospitali kuchunguzwa kama vile vipigo alivyokua akipewa viliweza kumuathiri ndani, kwa maelezo yake yeye ni kwamba alikua anapigwa kwa ubapa wa panga”
.
.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...