Sunday, January 22, 2012

MSANII ANASWA KWA UKAHABA



MREMBO mwenye mvuto wa kimahaba, Evonia William, juzi Jumatano alipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Sokoine Drive, Dar es Salaam kwa kosa la kufanya biashara haramu ya ukahaba.

Awali, mrembo huyo aliwahi kutupa karata yake kwenye ulingo wa filamu za Kibongo kwa kushiriki sinema tatu (scene chache) lakini ‘akalamba galasha’.

KUTOKA MAHAKAMANI
Mwendesha mashitaka wa mahakama hiyo, Richard Magodi alimsomea Evonia shitaka lake mbele ya Hakimu Mkazi, William Mutaki na kumwambia kuwa kosa alilokutwa nalo ni la kukaa eneo la wazi na kufanya ukahaba.

Mwendesha mashitaka huyo aliiambia mahakama kuwa, Januari 17, mwaka huu, saa 2:00 usiku, mshitakiwa huyo alinaswa eneo la Buguruni karibu na Baa ya Kimboka akifanya kosa hilo.

AKANA SHITAKA
Evonia alikana shitaka hilo na kumwambia hakimu kuwa alikamatwa eneo hilo kwa kosa la kupigana na changudoa aliyekuwa akijiuza, lakini yeye hakuwa na lengo la kufanya biashara hiyo.
Baada ya mrembo huyo kukana shitaka, mheshimiwa hakimu alimwambia kuwa, dhamana ipo wazi, lakini alikosa mdhamini hivyo alipelekwa rumande.

AMWANGUSHIA LAWAMA BABA YAKE
Mshitakiwa huyo akiwa mahakamani hapo, alimlalamikia baba yake mzazi aliyemtaja kwa jina la William Molo, kuwa ndiye chanzo cha yeye kuteseka na kuzurura hovyo.
Alisema, baba yake pamoja na uwezo wake mkubwa kifedha, alikataa kumsomesha, ndiyo sababu anahangaika mitaani.

“Kama baba yangu angenisomesha, nisingekuwa hivi. Ningekuwa na maisha mazuri kama mabinti wengine. Nimembembeleza sana anisomeshe lakini hataki. Akitokea msamaria yeyote kunisomesha au hata kufanya kazi za ndani, nipo tayari kutulia,” alisema msichana huyo huku akiangua kilio.
Kesi hiyo itatajwa tena Januari 31, mwaka huu mahakamani hapo huku Evonia akiendelea kula msoto rumande.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...