Tuesday, October 2, 2012

IMEVUJA: WEMA SEPETU HUIFICHA MIAKA YAKE HALISI ILI AWANASE WANAUME




Ijumaa ya last week 28th Sept ilikuwa ni birthday ya Wema Sepetu, hakuna asiyemfahamu kutokana na kuandikwa kila kukicha katika magazeti na blogs  au  webs  kutokana na mambo mbali mbali yakiwemo ya mahusiano aliyokuwa nayo na star mwenzake Diamond Platnums na mengineyo.

Katika siku yake ya kuzaliwa hiyo Ijumaa ilisemekana Wema ame ametimiza miaka  22..kwa maana kwamba alizaliwa 28th Sept, 1990. Sawa hilo hata sisi kwetu lisingekuwa na tatizo kabisa sababu huwezi uka judge age ya mtu kama ni kutoka kwake mwenyewe.

Lakini utata katika hili swala ukaanza kujileta kutokana na records ambazo tayari zipo na zinazofanya issue hii iwe na mkanganyiko.
 Issue kubwa ni kwamba Wema tayari yupo katika orodha ya walimbwende walioisha wahi kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Miss World kutokana na yeye kufanikiwa kulinyakua taji la Miss Tanzania mwaka 2006.


Sasa kama alishinda taji la miss Tanzania mwaka huo 2006 takriban miaka 6 kutoka leo, JE, hiyo inamaanisha mwaka huo alioshinda taji hilo alikuwa ana miaka 16?? Kama ndio, hili linawezekana vipi binti aliye chini ya miaka 18 kuruhusiwa kushiriki mashindano hayo? 
Na mbaya zaidi akashinda taji na kuiwakilisha nchi katika mashindano ya dunia


Kama vile haitoshi mapema mwaka huu Wema alifanyiwa Interview na Salama Jabir katika show inayozidi kupata umaarufu kwa sasa yaMKASI
Moja ya maswali aliyoulizwa Wema ni kuhusu lini alianza kujihusisha na mambo ya mapenzi, na jibu lake lilikuwa alipofikisha miaka 18. 
Salama alionesha kutaka kujua zaidi na akamuuliza tena ni lini alifikisha miaka 18, mrembo wema alisita kidogo na kumwonesha Salama kama anaogopa kusema bt end of da day akasema ni kama miaka 5 iliyopita, jibu lililomshtua Salama kidogo lakini akalipotezea na kuendelea na mengine.


Hiyo ni Interview ya mwaka huu 2012, na kama alidai kaanza mahusiano miaka 5 iliyopita that means kwa mujibu wa jibu la wema basi alitimiza  miaka 18 mwaka 2007, ambayo bado inathibitisha alishiriki mashindando ya Miss Tanzania 2006 akiwa under 18. Je, aliudanganya  umma ili aweze kuruhusiwa kushiriki? .

Baada ya story hizo za wema kutimiza miaka  22 Ijumaa iliyopita watu mbalimbali walianza kuhoji maswali juu ya umri huo huku wakioanisha na mwaka alioshinda taji la miss Tanzania. haya ni baadhi ya maoni ya watu kuhusu swala hilo kupitia Jamii Forum siku ya jana: 
--------------------------------------------------------------------------

TANMO, 30th September 2012, 20:37

How Old is Wema Sepetu?
Nimesoma mahali kwamba siku chache zilizopita huyu mdada ametimiza miaka 22, yet mwaka 2006 alishiriki shindano la kumtafuta Miss Tanzania, na akatwaa hilo taji hivyo akawakilisha jina la Tanzania kwenye mashindano ya dunia.. 
Sasa kama amezaliwa mwaka 1990 ina maana mwaka 2006 alikuwa na umri wa miaka 16 (under 18)... Ilikuwaje akaruhusiwa kushiriki haya mashindano na umri ule? Au yeye mwenyewe ndiye ameamua kujipunguzia miaka?

King Kong III, 30th September 2012, 20:37
Za kuambiwa changanya na za kwako

King'asti, 30th September 2012, 20:56
Wewe, umri wa mwanamke saa zingine unagota. Usishangae nikikualika besdei ikiwa na miaka minus 3 hapo mwakani. Ni nature.
Kafufue lile gazeti letu la umbea, nna hamu ya kusutwa!

30th September 2012, 21:11 Concrete
Mwaka 2006 alikuwa na miaka 20, mwaka huu atakuwa na miaka 26.

Hizo birthday ni promo za kuvutia wanaume tuu ili wamuone bado kigori kumbe anakaribia menopause.
Ila amechoka mbaya, yaani hapo bado hajaolewa na bado hajazaa watoto.

King'asti ,30th September 2012, 21:36
 sasa menopause ni leo? Hehehe, mjini kugumu jamani. Who doesnt want to be considered young? Mie mwenyewe im 21, ila unamkumbuka basila mwanukuzi?

30th September 2012, 22:05King Kong III
Mie tena nisimkumbuke Basila Mwanakuzi?? Miss Tanzania wa 1998

Sal, 1st October 2012, 14:48 
She's 22. Alisoma darasa moja na mdogo wangu ambaye wamezaliwa wote 1990.
Alidanganya umri, sababu ya urefu akakubalika.


--------------------------------------------------------------------------
Mpaka tunakwenda mitamboni jitihada za kumpata Mr Hashim Lundenga wa Lino Agency ambao ndio wandaaji wa mashindano ya Miss Tanzania kutaka kujua mwaka 2006 ilikuwaje Wema akashiriki katika shindano na kushinda taji hilo ilihali alikuwa under 18 (kama ni kweli), zimegonga mwamba kutokana na simu yake kutopokelewa kwa takribani masaa mawili.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...