Wednesday, May 9, 2012

UWOYA AMFANYIA BETHIDEI MWANAYE KRISH NDIKUMANA


Mtoto Krish akifurahia jambo.

Muigizaji Tino akiwasha mishumaa.

Baadhi ya watoto yatima wakiimba wimbo wa ‘Happy Birthday’.

Krish na mama yake wakizima mishumaa.

Krish akisaidiwa na mama yake kukata keki.

Uwoya akimlisha kipande cha keki mtoto wake.

Uwoya akitoa hotuba.

Watoto yatima wakiwa na Uwoya, Mariamna Krish.

Uwoya akikabidhi msaada wake kwa katibu mkuu wa kituo hicho cha CHAKUWAMA.

ICON wa filamu nchini, Irene Uwonya jana usiku wa Mei 8 aliandaa bonge la siku ya kuzaliwa mtoto wake wa kiume, Krish Ndikumana, akiwa ametimiza umri wa mwaka mmoja tangu azaliwe.
Krish ni mtoto wa mwanasoka raia wa Rwanda, Hamad Ndikumana ‘Kataut’.

Sherehe hiyo ilifanyika katika kituo cha watoto yatima cha CHAKUWAMA kilichopo Sinza-Mori jijini Dar.

Akizungumza na mtandao huu, mama wa mtoto huyo, Irene Uwoya, alisema amefarijika sana kufanya sherehe ya mwanaye akijumuika na watoto yatima kwani ameona ni moja ya kuwahakikishia watoto hao kuwa jamii inawajali.

“Sikutaka sherehe hii ya mwanangu niifanye katika ukumbi na kualika watu wengi ili waje kunywa na kula huku nyinyi watoto wenzake mkiwa mpo, kwani hiyo haitokuwa vizuri kwa upande wangu,” alisema Uwoya.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...