Saturday, March 17, 2012

MKE MJAMZITO AFUMWA AKILA URODA KWENYE BAJAJI




*ALIKUWA AKIFANYA NGONO KWENYE BAJAJ
*ANA MIMBA YA MIEZI 8, ALIA KWA KUOMBOLEZA
NI aibu iliyoje? Mke wa mtu ambaye ni mjamzito wa takribani miezi nane, amefumwa laivu akifanya uchafu na njemba ndani ya Bajaj...

Tukio hilo la kuhuzunisha kwa kiumbe alichokuwa nacho tumboni, lilinaswa na mapaparazi wetu pembeni mwa Barabara ya Kaijenge, Kijitonyama jijini Dar es Salaam, usiku wa kuamkia Alhamisi wiki hii...

SAA 6:30 USIKU
Mapaparazi wetu, wakiwa kazini saa 6:25 usiku, katika hali isiyokuwa ya kawaida waliona Bajaj ikiwa imeegeshwa pembeni mwa barabara chini ya miti huku ikiwa na watu ndani.

Baada ya kuitilia shaka, waliifuata na walipoikaribia walishuhudia ikitikisika huku kukiwa na miguno ya watu waliokuwa wakivunja amri ya sita (kuzini).

WAKURUPUSHWA
Walipoifikia Bajaj hiyo, waandishi wetu walipigwa na butwaa kumshuhudia mwanamke huyo akiwa na tumbo kubwa akifanya tendo hilo na njemba ambapo wawili hao walikurupuka na kuanza kutoka nduki huku wakiacha baadhi ya nguo.

Pamoja na kupigwa picha wakiwa ‘ovyo’, mwanaume alimshinda mwanamke kasi ya kukimbia hivyo kutokomea kusikojulikana lakini mwanamama huyo alishindwa kutokana na ‘kuchoka’ kwa ujauzito.

MAHOJIANO
HOT POT lilimuweka ‘mtukati’ mwanamke huyo ambapo mahojiano yalikuwa hivi;
HOT POT: Mama jina lako nani, unaishi wapi na ulikuwa unafanya nini na huyo mwanaume kwenye Bajaj?
Mwanamke: Siwezi kuwatajia jina wala sehemu ninakoishi kwa sababu ninyi siyo polisi, kwanza mniambie ninyi ni nani ndiyo nitawajibu maswali yenu.

HOT POT: Sisi ni waandishi wa habari, kwa hiyo tunaamini utatujibu maswali yetu.
Mwanamke: (huku akilia kama mtu anayeomboleza msibani) Jamani naombeni mnisamehe, mimi ni mke wa mtu, nimeolewa, mume wangu amekwenda kulala msibani Kigamboni (Dar), tumefiwa, mkiweka picha gazetini mtaniumbua…

HOT POT: Kwani mlikuwa mnafanya nini kwenye Bajaj na yule mwanaume ni nani?
Mwanamke: Sijui chochote, hapa nilipo nimeshachanganyikiwa.

Baada ya kushindwa kuzungumzia tukio hilo la aibu huku akiangua kilio, mwanamke huyo alisimamisha Bajaj nyingine iliyokuwa ikikatiza, akadandia na kutokomea kusikojulikana.

NI KAMCHEZO KALIKOZOELEKA
Hata hivyo, HOT POT hili lilizungumza na mlinzi anayelinda jirani na eneo hilo ambapo alithibitisha kuwa maeneo hayo yamekuwa na matukio mengi ya sampuli hiyo...

“Mbona kwenye Bajaj ndiyo mchezo wao? Achilia mbali wanaofanyia kwenye magari, hivi juzi tu hapa kuna jamaa wa bodaboda alikuja na mwanamke wakafanyia uchafu wao juu ya pikipiki ya matairi mawili,” alisema mlinzi huyo huku akikataa kutaja jina.

Saa kadhaa bila mwenye Bajaj kutokea, mapaparazi wetu waliondoka eneo la tukio na kumwacha mlinzi huyo akilinda usafiri huo uliogeuzwa kitanda cha sita kwa sita.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...