Friday, December 9, 2011

MAHABA: Ukiwa mbali na mpenzi wako, mezea lakini jua unasalitiwa!!



NI wiki nyingine tena tunakutana kupitia safu hii nikiamini kwamba umzima na unaendelea vyema na majukumu yako ya kila siku kama kawaida. 

Mimi namshukuru Mungu kwa kila ambacho amekuwa akinitendea katika kila siku ya maisha yangu. 

Nimshukuru pia kwa kunipa uwezo wa kuandika mada ambazo zimekuwa zikiwagusa wengi na kuwapa amani katika maisha yao ya kimapenzi.

Wiki hii msomaji wangu nitazungumzia mada ambayo naamini itawakosesha raha baadhi ya watu lakini sina jinsi, nalazimika kuiandika nikiamini itakuwa ni yenye manufaa kwa walio wengi. 

Ifike wakati tuambiane ukweli tu ili tujue namna ya kukabiliana na hali halisi.

Tunapozungumzia uhusiano wa kimapenzi, tunazungumzia watu kuwa pamoja na kushirikiana katika kila jambo linalogusa maisha yao. Hata hivyo, watu wanaweza kutokea kupendana lakini yakajitokeza mazingira ambayo yanawalazimisha kuishi mbalimbali.

Wapo waliooana lakini kazi au sababu nyingine zimewafanya waishi mbalimbali. 

Kuna wachumba na wapenzi wa kawaida ambao kutafuta maisha kama vile kazi na elimu vimewafanya waishi maeneo tofauti. 

Unakuta huyu yuko Tanga, mwingine yuko Arusha. Huyu yupo Tanzania mwingine yuko Marekani lakini wanapendana na hakuna aliye tayari kumkosa mwenzake.

Katika hili, ninachotaka kukizungumzia ni hii kasi ya wapenzi wanaoishi mbalimbali kusalitiana. 

Katika mapenzi ya kweli hakuna suala la kusalitiana, kila mmoja atajitahidi kuvumilia na kuhakikisha anavishinda vishawishi ili asigawe penzi kwa mtu mwingine.

Lakini sasa kuna mazingira flani ambayo yakiwepo kusalitiana kunakuwa na asilimia kubwa kutokea. Juzi nilibahatika kuzungumza na dada mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Fauzia.

 Yeye anasoma Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na mchumba wake aliyemtaja kwa jina moja la Juma anasoma Uganda.

Dada huyu anasema: “Tulikuwa tunapendana sana, alikuwa ananipa mapenzi ambayo sijawahi kuyapata, aliniahidi ndoa akanivisha pete lakini huku tunakoelekea naona kabisa hatutafikia ndoto zetu.

“Yeye yuko Uganda na mimi niko Dar lakini taarifa niliyopewa na ndugu yangu aliyepo chuoni hapo ambaye hawajuani ni kwamba, mchumba wangu huyu ana mtu mwingine huko na wamekuwa wakionekana maeneo wakiponda raha.

“Naumia sana kwani kila nikimpigia simu na kumuuliza juu ya hilo ananiambia, hayo ni maneno ya watu wasiopenda kutuona tunapendana. Eti ananiambia hana mwingne anayempenda zaidi yangu lakini huku naambiwa ana mtu mwingine.”

Hilo limemtokea Fauzia lakini ninachoamini ni kwamba hayo ndiyo mazingira yanayojitokeza kwa wapenzi wengi wanaoishi mbalimbali. Uvumilivu na uzalendo vimekuwa vikiwashinda wengi. 

Mpenzi wako anaweza kuwa mbali na wewe na akakuahidi kutokukusaliti lakini akiwa huko akakusaliti bila hata wewe kujua, lakini watu wanaoujua uhusiano wenu wanabaki kukuonea huruma.

Ni suala lisilo na ubishi kwamba hisia ni kitu kigumu sana kukizuia, unaweza kumuuliza mtu kwamba, anawezaje kukabiliana na hisia zake wakati mpenzi wake yuko mbali?

 Jibu atakuambia eti akijiwa na hisia hizo anajiweka bize na mambo mengine. 

Ni kweli wapo wanaoweza kufanya hivyo lakini wengi wanaishia kusaliti tena wengine huku mioyo yao ikiwauma.

Mioyo yao inawauma na roho zao zinawasuta kwa kuwa wameshawaahidi wapenzi wao kuwa hawatawasaliti lakini wanafanya hivyo kwa sababu ya tamaa zao.

 Usaliti unakujaje?
Kwanza ifahamike kwamba, kama mpenzi wako yuko mbali sana na wewe na mnakaa kwa muda hata wa miezi sita na zaidi bila kuonana, kusalitiwa kuna asilimia nyingi ila unachotakiwa kukifanya ni kumuamini tu mpenzi wako. 

Unatakiwa kumuamini tu kwa kuwa, kwanza ni vigumu kubaini kuwa anakusaliti na hata ukimuuliza atakuambia hawezi kukusaliti lakini kumbe inawezekana hata muda huo wakati mnaongea yuko na mtu mwingine kitandani.

Iko hivi, kama mpenzi wako yuko masomoni, elewa huko aliko atakutana na mtu mwingne ambaye naye mpenzi wake hayuko naye. 

Hawa wataanzisha urafiki wa kwaida, watapeana kampani za hapa na pale lakini hawa wanayo nafasi kubwa ya kuwasaliti wapenzi wao, na hiki ndicho kinachotoea kwa wengi.

Hilo liko sana vyuoni na makazini hivyo kama mpenzi wako yuko mbali na wewe kwa sababu ambazo hazizuiliki, unatakiwa kuwa na moyo wa uvumilivu au utakiwa kuwa ni mtu wa kupotezea sana laa sivyo unaweza kujikuta unaachana na mtu ambaye ulitokea kumpenda sana.

Kujizuia ni vigumu?
Wapo wanaoweza kukabiliana vilivyo na tamaa zao, hawa ni wale wachache wanaowaheshimu wapenzi wao, wanaoweza kutafuta njia mbadala za kuziridhisha nafsi zao pale hisia za kufanya mapenzi zinapowajia. 

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...