Sunday, November 27, 2011

FABOLOUS, INTER COLLEGE BASH ILIVYOBAMBA!!!


                                   Fabolous akifanya makamuzi.
..Sehemu ya nyomi iliyohudhuria


Juma Nature na kundi lake la Wanaume Halisi.


SHOO ya Inter College Bash iliyokuwa inahusisha vichwa makini kutoka nchini Marekani na hapa Bongo, usiku wa kuamkia leo ilifana vilivyo katika viwanja vya Leaders Kinondoni jijini Dar es Salaam, ambapo Fabolous aliweza kupiga shoo iliyochukua zaidi ya dakika 30 wakati wazawa wakitumia zaidi ya saa nane. Mbali na Fabolous ambaye ilikuwa kawaida kwake kufanya vizuri, wasanii wa Bongo waliosisimua mioyo ya mashabiki wao ni Juma Kassim ‘Juma Nature’ na kundi zima la Wanaume Halisi, Seleman Msindi ‘Afande Sele’, Wanaume Family, Haroun Kahena ‘Inspector Haroun’ akiongoza kundi zima la Gangwe Mob. Wengine ni Hamisi Mwinjuma ‘Mwana FA’, Jay More, Nako 2 Nako, Joe Makini , Niki wa Pili, Elias Barnaba, Manzese Crew, Kikosi cha Mizinga kikiongozwa na Kala Pina na THT Dances.
Selemani Msindi 'Afande Sele' akiwa kazini.


Kiongozi wa kundi la Gangwe Mob Haroun Kahena ‘Inspector Haroon’ (kushoto), akionyesha uwezo wa kundi hilo na mwenzake Luteni Kalama.


Naseeb Abdul ‘Diamond’ akiwajibika.


Msanii wa muziki wa kizazi kipya Bongo ‘Hamisi Mwijuma ‘Mwana FA’ (kulia), akitoa burudani na msanii mwenzake, Shetta.


Joe Makini naye hakuwa nyuma kutoa burudani.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...