Tuesday, November 22, 2011

DUNIA IMEKWISHA: Binti abakwa na baba yake kwa miaka 13 mfululizo...





Mtuhumiwa ambaye ni baba mzazi wa binti huyo, bwana Muzamil Said.
KUNA watu wanasema dunia imevaa sketi ndiyo maana wanaotakiwa kujenga ndiyo hao hao waharibifu. Baba bila soni, kavua nguo mbele ya mwanaye wa kike, akambaka. Hakukoma, akaendelea tena na tena.

Ni madai mazito yaliyopo polisi. Binti mwenye umri wa miaka 16 (jina tunalo), anamtuhumu baba yake mzazi, Muzamil Said kwa kumbaka mfululizo.

Shauri lipo Kituo cha Polisi Mbagala, jalada lina kumbukumbu namba MBL/RB/10719/2011 KOSA LA KUBAKA.
Kwa mujibu wa binti huyo, baba yake alianza kumbaka tangu akiwa na kadirio la miaka mitatu mpaka mwaka huu mchezo huo ulipobainika. Kwa hesabu hizo, ni wazi alitendwa ukatili huo kwa miaka 13.

MCHEZO ULIVYOANZA
Binti huyo, anaishi na baba yake Mbagala, eneo la Nzasa B, anasimulia: “Nakumbuka nilikuwa kama na miaka mitatu hivi, baba na mama yangu mzazi walitengana. Tangu wakati huo, sijamuona tena mama yangu kwa maana aliondoka moja kwa moja.

“Baada ya hapo tulianza kuishi wawili, mimi na baba tu. Ni kipindi hicho baba alianza kunibaka, nilikuwa napata maumivu makali lakini yeye aliendelea. Ikafikia hatua nikawa siwezi hata kuzuia mkojo. Nikibanwa tu najikojolea.
Binti ambaye amekuwa akibakwa na baba yake kwa takribani miaka 13.
“Ikafika kipindi, baba akamtafuta mama mwingine (mama wa kambo), tukawa tunaishi wote lakini mara kwa mara usiku baba alimtoroka huyo mama na kuja kunibaka.

“Mwezi huu ndiyo mama aligundua, kwani kama kawaida yake, baba alimtoroka na kuja kulala kwangu. Baadaye mama alikuja kimya kimya na kumkuta akiwa ananibaka. Mama akamgombeza baba kwa kilugha.

“Mama akaniuliza ile tabia imeanza lini? Nikamueleza kila kitu. Nikamfafanulia na jinsi nilivyo na tatizo la kutokwa na mkojo. Mwanzoni baba aliniambia eti akiniingilia mara kwa mara tatizo la mkojo litaisha lakini nimebaini kuwa si kweli, kwani linaendelea mpaka leo.

“Nilikuwa nasoma Shule ya Msingi (jina kapuni), darasa la tano lakini nimeacha kwa sababu sipo sawa. Tatizo la kukojoa linaendelea na akili yangu pia imevurugika.”

KAULI YA MWENYE NYUMBA
Alhaj Abdilah Mohamed Mwahu ndiye mwenye nyumba wa Muzamil na hili ni neno lake: “Huyo binti alikuja kunilalamikia, ikabidi niwashirikishe wapangaji wengine, mwisho tukakubaliana tumuokoe binti kwa kulifikisha suala lake kwenye vyombo vya sheria.

“Tulianzia serikali za mitaa kabla ya kupeleka shauri Kituo cha Polisi Mbagala. Polisi walimkamata lakini akaachiwa kwa dhamana, na sasa hatujui alipo.”

SERIKALI YA MTAA, NZASA B
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa, Nzasa B, Jeruin Mkude alisema: “Suala hilo lipo lakini polisi hawanipi ushirikiano.”
UTAMU imebaini kuwa, shauri la Muzamil limeganda polisi, kwani tangu baba huyo alipopewa dhamana, mpaka sasa hajarudi kuripoti na hajulikani alipo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...