Sunday, January 29, 2012

Wema aonesha jeuri ya fedha..




SUPA staa wa Bongo, Wema Isaac Sepetu juzikati alionesha jeuri kubwa ya fedha pale alipomwaga minoti jukwaani akiwatuza wanamuziki wa Bendi ya Mapacha Watatu...

Tukio hilo lilitokea Januari 24, mwaka huu ndani ya Ukumbi wa Star Coco Beach, Dar ambapo bendi hiyo ilikuwa ikitumbuiza.

Awali, wakati nyota huyo anaingia kwa mbwembwe, mwimbaji wa bendi hiyo, Kalala Hamza ‘Junior’ alipeleka kinywa kwenye ‘maiki’ na kumtaja jina hali iliyowafanya mashabiki wageuke kumwangalia.

Hapo sasa, Wema alikwenda moja kwa moja jukwaani na kutoa minoti kisha kuimwaga chini kama majani yanavyopukutika kwenye mti baada ya kukauka.

Noti hizo ambazo paparazi wetu alizihesabu kwa harakaharaka wakati zikiokotwa, zilizunguka kwa wanamuziki wote wa bendi hiyo.

Baadaye mwanamuziki wa Bendi ya Mashujaa, Charles Gabriel ‘Chaz Baba’ alipanda kuimba kama mwalikwa, na yeye alikutana na ‘mvua’ hiyo ya pesa hadi aliposhuka.
Hali hiyo iliendelea kila mara, mpaka baadhi ya mashabiki wakampachika staa huyo jina la pedeshee wa kike Bongo.


Wema alilikubali jina hilo na baadaye akaanza kujiita mwenyewe.
Mpaka anaondoka ukumbini hapo, Wema licha ya kwamba alikuwa ‘chicha’ kwa ulabu, pia aliendelea kujiita pedeshee wa kike huku akiwa ameshatumia shilingi laki tano za Kitanzania.

“Mimi ni pedeshee wa kike Bongo. Leo nimefikisha sadaka yangu kwa watu,  maana hata Mungu anasema unapojua kupokea basi jua na kutoa kwa wenzako. Sasa hivi mimi pesa ninayo bwana, nina akaunti mbili, moja ya pesa ya Tanzania nyingine dola,” alisema Pedeshee Wema. 

Saturday, January 28, 2012

Kizaazaa cha Mchina!!!!





Dawa za Kichina za kuongeza makalio zimeleta kizaazaa cha aina yake kufuatia baadhi ya wanawake waliozitumia kwa lengo la ‘kuwachanganya’ wanaume kukiona cha mtemakuni.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa, baadhi ya wanawake hao wakiwemo mastaa wa Bongo sasa wanahaha kutafuta njia za kupunguza miili yao baada ya kubaini uamuzi waliochukua awali haukuwa sahihi.
Imebainika kuwa, kufuatia matumizi ya dawa hizo wapo ambao sasa hawatamaniki kutokana na kuwa na maumbile ‘kichekesho’ hivyo kukosa ule mvuto waliotarajia.
Akizungumza kwa masikitiko, mwanamke mmoja aliyeonekana kuathirika na dawa hizo aitwaye Zaina wa Kinondoni, Dar alisema, awali alidhani kuwa na makalio makubwa kungesaidia kumdatisha mumewe lakini kumbe ndiyo alikuwa anatafuta matatizo.
“Nilikuwa na umbo langu zuri tu, wenyewe wanaita namba nane lakini shoga yangu akanishawishi nitumie dawa hizo akidai eti nitakuwa na kalio litakalomdatisha mume wangu, kumbe ndo’ kaniingiza mkenge.
“Ona nilivyo, kwa kweli najuta kutumia dawa hizi, hapa nilipo nimeambiwa kuna dawa inaitwa Mlonge inayotibu magonjwa mbalimbali, ndio naisaka ili niondokane na hali hii,” alisema mama huyo.
Naye Husna wa Magomeni aliliambia Risasi Jumamosi kuwa, yeye alikuwa akitamani kuwa na kalio kubwa na akashauriwa na marafiki zake atumie dawa hizo za Kichina lakini kwa anachokiona kwa dada yake, hataki kabisa kuzisikia.

“Dada yangu hatamaniki kwa dawa hizo. Alikuwa na umbo zuri lakini baada ya kuzitumia, amekuwa kituko na kila alipopita amekuwa akipata usumbufu kutoka kwa wanaume,” alisema Husna na kuongeza:
“Mbaya zaidi kumbe mume wake alikuwa hapendi mwanamke mwenye wowowo, sasa hivi hakuna maelewano ndani ya ndoa na mume wake amekuwa akimsaliti kwa kwenda kutafuta dogodogo nje, mimi sitaki kuingia huko.”
Tabia ya baadhi ya wanawake kutumia dawa za kuongeza makalio kama wanavyoonekana wanawake walio ukurasa wa mbele imekuwa ikiwaletea matatizo ikiwa ni pamoja na wengine kushindwa kuwajibika vilivyo wawapo faragha na wapenzi wao na kuzomewa wanapokatiza mitaani.
BLOG hii linawashauri wanawake kukubaliana na maumbile waliyopewa na Mungu kwani kutafuta muonekano mpya kwa kutumia dawa hizo na nyinginezo ni kujitafutia madhara yanayoweza kuathiri maisha yao.

Maskini vengu... Taarifa toka INDIA inasikitisha...





HALI ya msanii ‘jembe’ wa Orijino Komedi, Joseph Shamba ‘Vengu’ (pichani) imeelezwa bado ni tete huku kauli mbiu ikiendelea kuwa ileile ‘jamani tumuombeeni Vengu.’

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa Mtanzania mmoja anayefuatilia afya ya staa huyo nchini India alipo kwa matibabu, hali si nzuri licha ya kukutana na madaktari bingwa wa huko.

“Jamani cha kusisitiza ni kwa Watanzania huko nyumbani tuzidi kumwombea Vengu, bado hayuko vizuri, hali ni tete,” alisema Mtanzania huyo kwa kuweka mada kwenye Mtandao wa Kijamii wa Facebook.


Baada ya taarifa hiyo ya kushtua, Jumanne wiki hii, mapaparazi wetu walitinga nyumbani kwa msanii huyo, Mabibo jijini Dar es Salaam ili kusikia chochote kutoka kwa familia yake.

Awali, mapaparazi wetu walizungumza na jirani mmoja aliyekataa kutaja jina lake ambapo alisema anachojua yeye, msanii huyo atarudishwa Tanzania ili familia ijaribu na dawa za mitishamba.

“Msiniulize sana mimi, kwao pale (akisonza kidole kuwaonesha mapaparazi wetu). Ila nasikia watamrudisha ili wajaribu dawa za mitishamba. Nasikia hali si nzuri,” alisema jirani huyo mwanamke.

Mapaparazi wakakanyaga hadi nje ya nyumba ya akina Vengu na kukutana na dada mmoja ambaye awali alisema pale sipo kwenye makazi ya msanii huyo, lakini alipobanwa sana alikiri.
“Haya, hapa ni kwa akina Vengu, mnasemaje?”

Utamu: Lengo letu kujua hali ya Vengu, anaendeleaje? Maana tumesikia hali ni mbaya kule India?
Dada: (bila kutaja jina lake) Vengu anaendelea… vizuri, lakini Watanzania wazidi kumuombea sana.
Licha ya jitihada za mapaparazi wetu kutaka kumdadisi zaidi, dada huyo alisema  yeye si mzungumzaji na kusema kama zinahitajika taarifa zaidi ya hapo basi kaka mkubwa wa familia ndiye anawajibika kwa hilo, lakini hakuwepo nyumbani muda huo.

KUNA SIRI INAENDELEA?
Siku hiyo mapaparazi wetu walipofika nyumbani kwao na staa huyo, mwanamke mmoja aliyeonekana ndiye mama mzazi wa Vengu alikuwa ndani amejiinamia wakati dada huyo akizungumza.
Mapaparazi walipomuuliza mwenyeji wao kama mwanamke huyo ni mama wa Vengu, alisema siye, ni mgeni alifika pale kusalimia tu.
Utamu: Tunamuomba nje tuongee naye basi.
Dada: Hakuna, haiwezekani.

KUMBUKUMBU NDEFU
Vengu, awali alilazwa kwa muda mrefu kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) akikabiliwa na ugonjwa uitwayo kitaalam Brain au Cerebral Atrophy ambapo seli za kichwani hukosa mawasiliano na sehemu nyingine, pia mgonjwa hupoteza fahamu.
Hali ilipozidi kuwa tete, ‘komediani’ huyo alipelekwa Hospitali ya Apolo nchini India kwa matibabu zaidi.

Imesharipotiwa kwamba ili msanii huyo apone sawasawa matibabu yake yatagharimu shilingi milioni 320 za Tanzania.
KUTOKA KWA MHARIRI
Wapo Watanzania wengi wenye karama za maombi hata mgonjwa akiwa mbali, ni nafasi nzuri wakafanya hivyo kwa Vengu na wasanii wengine ambao hawana majina makubwa. Mungu awaponye wote. Amina.

Friday, January 27, 2012

AISHA MADINDA YUKO HOI ...




MNENGUAJI wa Bendi ya Extra Bongo ‘Wazee wa Kizigo,’ Aisha Mohammed Mbegu ‘Aisha Madinda’ (pichani) yuko hoi tena akisumbuliwa na tatizo lilelile la kuvimba miguu.


Akizungumza nyumbani kwake Kinondoni Mkwajuni, Dar es Salaam huku afya yake ikionekana kudhoofika sana, Aisha alisema ni takribani mwezi wa pili sasa hajapanda jukwaani kutokana na hali aliyonayo.


Alisema kinachomchanganya zaidi ni kwamba amekwenda hospitali mbalimbali lakini tatizo halijaonekana zaidi ya kupewa dawa za kupunguza maumivu na kutakiwa kurudi nyumbani.
“Hali yangu kwa kweli siyo nzuri kabisa, miguu imevimba tena kiasi cha kinikosesha amani. Nimekwenda hospitalini wameniambia hawajaona tatizo ila wakanipa dawa flani ambazo nimetumia na sasa kidogo huu mguu moja umepungua ila huu mwingine bado,” alisema Aisha.


Akaongeza kuwa, kwa hali aliyonayo anaamini ni mambo ya dunia hivyo akawaomba mashabiki wake wamuombee dua ili apone na arudi jukwaani kuwapagawisha.
 “Kikubwa mashabiki wangu waniombee, nina imani nitapona na kuondokana na mateso haya,” alisema Aisha ambaye mara kwa mara amekuwa akisumbuliwa na tatizo hilo.

KIMENUKA... WEMA, KAJALA WAGOMBEA BWANA...



http://api.ning.com/files/v864S1k6upToZ0emQVN2OKNteDAr7*RTYRd59YJ-d0COBm8rzsqlCtO8-6wgFoDvuPyFIRql0RMhoufytkdPCNWTF7RvTXf2/kajalal.jpg
Kajala Masanja.
Wema.
KIMENUKA! Wema Isaac Sepetu na Kajala Masanja, wanadaiwa kuingia kwenye bifu ‘babkubwa’ kisa kikidaiwa ni kugombea mwanaume...

NI KIGOGO WA IKULU
Kwa mujibu wa chanzo kisicho na shaka, hivi karibuni warembo hao ‘wanaokinukisha’ katika tasnia ya filamu Bongo, walijikuta wakiingia kwenye gogoro kufuatia Kajala kutuhumiwa ‘kumtokea’ mwanaume mpya wa Wema aliyetajwa kwa jina moja la Clemence ambaye anadaiwa ni kigogo wa Ikulu.

Chanzo hicho kilidai kuwa Wema alimtambulisha Kajala kwa mwanaume huyo mwenye noti zake tofauti na msanii Naseeb Abdul ‘Diamond’ aliyekuwa ‘akiminya’ na Miss Tanzania huyo wa mwaka 2006.

KAJALA ASAKA NAMBA YA GARI
Ilidaiwa kuwa, baada ya Kajala kutambulishwa kama shemeji, ulipita ukimya f’lani, nyuma kukiwa na madai kuwa alikuwa akisaka namba ya gari la jamaa huyo ili kumsaidia kufahamiana naye kabla ya kunasa namba yake ya simu.

“Asikwambie mtu, Kajala alipokosa namba ya simu, mwanzoni alikuwa akisaka mpaka namba ya gari, lakini Mungu si Athumani, alifanikiwa kupata ya kilongalonga ‘coz’ Wema aliachia mwanya fulani akijua ni shosti wake hivyo hawezi kufanya chochote.

“Kikulacho ki nguoni mwako, fumba fumbua Wema akapelekewa malalamiko na mwanaume kuwa Kajala anataka mambo,” kilidai chanzo hicho ambacho ni rafiki mkubwa wa wawili hao.

Chanzo hicho kiliendelea kudai kuwa, baada ya Wema kufikishiwa ushahidi wa ‘sms’, kama kawaida yake, hakuhoji chochote zaidi ya kumvaa Kajala mzimamzima na kukinukisha na sasa hawaivi.

PICHA YA JOKATE, DIAMOND
Huku kikilionesha ushahidi kwenye mtandao wa BBM, chanzo hicho kilidai kuwa ishu hiyo ilihamia kwenye mtandao huo ambapo Kajala aliweka picha ya Jokate Mwegelo na Diamond akiandika: “Chezea Hao!”

Ilisemekana kuwa, picha hiyo ilitoa nafasi kwa wadau wa mtandao huo kumtukana Wema kwa kuweka maoni ya matusi. Habari zilizidi kuweka kweupe kuwa, Wema aliposikia ishu hiyo, alizama mtandaoni humo na kujionea mwenyewe.

WEMA AJIBU MAPIGO
Ilielezwa kuwa, katika vitu ambavyo Wema huwa hapendi ni kusikia au kutajiwa ishu ya Jokate na Diamond hivyo naye akajibu mapigo.

Ilifahamika kuwa, Wema naye alitafuta picha ya bwa’mdogo anayedaiwa kutoka naye aliyetajwa kwa jina moja la Petty Man akiwa kimahaba na kidemu kingine kilichotajwa kwa jina moja la Hamisa, hivyo Kajala naye akapokea za uso laivu kutoka kwa wadau wa mtandao huo.

Hata hivyo, pamoja na hayo, ilidaiwa kuwa Kajala hakufanikiwa kumnasa mwanaume huyo kufuatia Wema kuweka ulinzi mkali na kuvunja ushosti wao.

MSAKO KUWEKA HESHIMA MJINI
Chanzo kiliendelea kusema kuwa, baada ya wawili hao kutifuana kwa maneno, sasa wanasakana ili kushikishana adabu na kuwekeana heshima mjini.

KAJALA ANASEMAJE?
Kama kawa, kama dawa, baada ya mtiti huo kutua kwenye dawati, mtu wa kwaza kutafutwa ili kuweka wazi anachokijua ni Kajala ambaye alikuwa na haya ya kusema:
“Duh! Kweli nyie mnatisha, mimi sina ‘comment’ muulizeni huyo Wema.”

HEBU MSIKIE WEMA
Alipotafutwa Wema na kumwagiwa ‘upupu’ mwanzo hadi mwisho, alikuwa na haya ya kusema:
“Siwezi kugombea mwanaume na Kajala, ila kuna kitu kilitugombanisha.
“Huyo Hamisa ni mdogo wangu wa hiari ‘so’ nina uhuru wa kuweka kitu chochote kwenye ukurasa wangu wa BBM.”

Alipotakiwa kueleza hicho kilichosababisha wakagombana, Wema hakuwa tayari, lakini HOT POT inaendelea na mchakato kujua kisa na mkasa kwani ndiyo muvi imeanza, kaa tayari.  

Thursday, January 26, 2012

MABADILIKO MAKUBWA NDANI YA FACEBOOK, KUWA MAKINI...



Picha inayoonesha muonekano wa Timeline ndani ya Facebook.

Facebook ikiwa ni nyumba ya online kwa mamilioni ya watu duniani, hivyo mabadiliiko yanayotokea kwenye facebook ni dhahiri yanaathiri wengi wetu. Katika siku za karibuni Facebook wamekuja na kitu kipya ambacho wenyewe wanakiitaTimeline, hii Timeline ni mpangilio mpya wa kurasa za facebook ambao unamuwezesha mtumiaji kupanga picha, matukio n.k kulingana na muda husika. 

Katika Timeline, utaweza kupanga taarifa zako kwa mtindo wa kipekee zaidi huku ukimpa nafasi mtembeleaji kuzipitia kwa haraka zaidi. Kama utaangalia picha ya hapo juu, utaona kwenye timeline mtu akija mara ya kwanza ataona marafiki, picha na mengine mengi. Siyo hayo tu, kwa kutumia Timeline mtu anaweza kuangalia matukio yako toka siku ya kwanza uliyojiunga na facebook.

Katika siku zilizopita Timeline ilikuwa ni kwa wanaohitaji, ila kuanzia tarehe moja mwezi wa pili Timeline itakuwa ni lazima, utake usitake ni lazima utumie au kwa lugha ya kiufundi tunaweza iita default. Hivyo usishangae kuona mabadiliko kwenye kurasa yako....

Kitu ambacho kimenivuta kuandika hii makala ni kuwa, ingawa Timeline ni nzuri na ya kuvutia, ila Facebook inaonekana wanazidi kufanya mambo kuwa magumu, ni dhahiri kuwa kufanikiwa kwa facebook kumekuja kutokana na urahisi wa utumiaji. Hivyo kufanya mambo kuwa magumu kutawafanya watu wengi kuikimbia au kushindwa kuifungua hususan wale walio kwenye mgao wa bandwith (internet zilizo taratibu mno). Kuna siku niliwahi kuona mpachiko wa rafiki yangu ambaye ni mtumiaji mzuri mno wa facebook, yeye alikuwa akilalamika kwa kusema nani amesema tunataka hii Timeline?

Kitu kingine kikubwa ambacho kinaniumiza kichwa ni privacy, facebook wenyewe mara kibao wamekiri kuwa privacy ni moja ya vitu vinavyowaumiza kichwa, kwenye facebook ya sasa mtu anaweza kuona matukio yako ndani ya wiki hadi mwezi, ila sasa kwenye hii Timeline mtu anaona tukio tangu siku ya kwanza uliyojiunga facebook, sasa  huku si kuwaumbua watu?  Chukulia mfano kwa wale wenzangu na mimi wazee wa kuongopa, huu si ndio mwanzo wa kukamatwa?  Hivyo basi kwa kuweka Timeline kuwa default kutawatatiza wengi. Habari njema ni kuwa kuanzia sasa unaweza kuanza kufuta matukio kadhaa usiyopenda kuwaonesha watu hadi hapo Januari 31!!!!

WATOTO WAWILI WAUAWA, WANYOFOLEWA VIUNGO VYA MWILI JIJINI MBEYA..



Mwili wa marehemu Silvia Isaya (5) aliyeuawa kisha viungo vya mwili wake kunyofolewa ulimi, jicho la upande wa kushoto, sehemu za siri na mguu wake wa kushoto kuvunjwa ukiwa umefunikwa kwa kitenge, kutokana na kuharibika vibaya hivyo kushindwa kuoneshwa.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Nsenga jijini Mbeya wakitoka kushuhudia mwili wa mwanafunzi mwenzao wa darasa la kwanza, Silvia Isaya (5) alieuawa kisha viungo vya mwili wake kunyofolewa ulimi, jicho la upande wa kushoto, sehemu za siri na mguu wake wa kushoto kuvunjwa.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Nsenga Bwana Gibson Mwaselela (mwenye koti la rangi ya Samawati ), Baadhi ya wananchi wa Nsenga jijini Mbeya wakishuhudia mwili wa mwanafunzi wa darasa la Kwanza Silvia Isaya (5) alieuawa kisha viungo vya mwili wake kunyofolewa ulimi, jicho la upande wa kushoto, sehemu za siri na mguu wake wa kushoto kuvunjwa.

WIMBI la mauaji dhidi ya watoto limezidi kutanda mkoani Mbeya baada ya watoto wawili kuuawa katika nyakati tofauti na watu wasiojulikana na kisha kunyofolewa baadhi ya viungo vya mwili huko Wilaya ya Rungwe na Mbeya.

Kufuatia tukio hilo jumla ya wananchi 14 walikamatwa na Jeshi la Polisi lakini machifu waliingilia kati, ambapo mtu mmoja aitwaye Joseph Mwangolobe (40 - 45) , mkazi wa Kiwira alijitokeza na kukiri kuwa ndiye aliyehusika na mauaji hayo chumbani kwake.

Jeshi la polisi lilifanya kazi ya ziada kumnusuru Joseph asiuawe na wananchi wenye hasira kali baada ya wananchi hao kutaka kulipiza kisasi, na familia yake imelazimika kuhama ikiwa chini ya ulinzi wa polisi.

Baba mzazi wa mtoto Silvia Isaya (5), Bwana Isaya Samson Mwalyego amesema alimwacha mwanawe Silvia majira ya saa 11:00 jioni Januari 13, mwaka huu alipokuwa anakwenda kazini Hoteli ya Silver Coin, wakati mama yake akienda kutafuta mahitaji ya nyumbani kwa ajili ya mlo wa usiku.

Mama mzazi alipomaliza kupika alimtafuta mwanae pasipo mafanikio hivyo alitoa taarifa kwa Mtendaji wa kijiji cha Nsenga, Bwana Meshack Mwaipasi ambapo walitafuta usiku huo bila mafanikio.

Asubuhi majira ya saa 2 kamili Januari 24, mwaka huu, mwili wa mtoto huyo ulipatikana katika shamba la mahindi Kitongoji cha Isenyela Kata ya Nsenga ukiwa umeondolewa baadhi ya viungo na mwili wa mtoto huyo ulichukuliwa na kupelekwa katika Hospitali ya Rufaa kwa uchunguzi zaidi.

Kamanda wa Polisi Advocate Nyombi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba uchunguzi unafanyika ili kuweza kuwabaini waliohusika na tukio hilo la kikatili.
 

Wednesday, January 25, 2012

BIG BROTHER AFRICA!!!! NEW GAME CALLS FOR PAIRS…



http://www.namibian.com.na/uploads/pics/BIG_BROTHER_AFRICA.jpg
BREAKING NEWS:
YOU CAN ENTER BIG BROTHER AFRICA BUT NOT ALONE!
NEW GAME CALLS FOR PAIRS…
January 2012
Just when DStv audiences thought that they had seen all the incredible twists and turns that mega-hit reality-TV franchise Big Brother Africa could possibly include, M-Net’s sensational series has pulled off another huge surprise.
And you know it’s a massive announcement when even the fact that this season’s brand new cash prize of a cool USD 300 000 isn’t the headline-grabbing news!
Grabbing that honor is the revelation from series producers that this season, entrants must DOUBLE-UP to compete. This means that anyone who wants to enter season 7 must partner with another person to enter as a pair!
So whether you enter with your best friend, boyfriend, girlfriend, mom, dad, brother, sister, boss, husband, wife, neighbor, hairdresser, whomever…you must just make sure that you enter as a pair. So who will take the journey of a lifetime with you? Remember you may have to spend a long time with them in the house so choose carefully!

PLUS, in another bold change, Big Brother Africa welcomes two new countries Liberia and Sierra Leone to the Big Brother house for the first time ever, while this time round, Ethiopia bows out of the game and Mozambique will take on a new role that will be announced at a later stage.

That means that this year, if you want to enter Big Brother Africa you can do so if you and your partner are citizens from one of the following participating countries: Angola, Botswana, Ghana, Kenya, Liberia, Malawi, Namibia, Nigeria, Sierra Leone, South Africa, Tanzania, Uganda, Zambia and Zimbabwe.

Both partners must come from the same country, must be 21 years or older, must be fluent in English and must have a valid passport.

Interested persons can collect an entry form from the nearest MultiChoice office in their country anytime from February 5. Alternatively you can also enter by logging on to www.mnetafrica.com/bigbrother and completing an entry form online. Or download an entry form from the website, complete and email it back to bba@endemol.co.za. All online entry forms will also be available from February 5. Whatever you choose to do, do it fast because the deadline for entries is February 27, 2012!

And remember that, as with previous seasons, entrants must be fun-loving, vocal, creative, original and articulate. In addition all entrants must the social flexibility to live in close proximity with others and must be tolerant of views and lifestyle choices other than their own.

Commenting on the surprise turn of events, M-Net Africa Managing Director Biola Alabi says, “We are thrilled to be offering a huge, new, USD 300 000 prize and to include two new countries who were chosen to participate based on their ongoing interest in the series and their growing DStv audiences.  And while Ethiopia won’t have a housemate this year, we’ll look to include them and other non-housemate countries in other ways if the opportunity arises, as we do every season. We are and have always been proudly committed to making this a truly African show. And as for Mozambique, they will be included with a housemate – but that’s all we are saying at the moment!”

She goes on to say, “Of course, the really big news this season is that entrants must enter as pairs. In the past we’ve seen a natural and continuous cross-over between individuals and their families, their friends. So this year, we decided to include that as part of the game. It will definitely make a dramatic addition to the series so we urge people to enter and experience what will be a uniquely different Big Brother Africa!”

So with just days to go until the official start of Big Brother Africa 7, start thinking about who you want to share this amazing adventure with. Then make sure you enter AS SOON AS POSSIBLE!

Produced for M-Net by Endemol South Africa, the new season of Big Brother Africa will be headline sponsored by Coca-Cola for the second consecutive year and will be screened to 47 countries across the continent, live 24/7 for 91 days on DStv channel 198. The series starts Sunday May 6.







Binti wa LIYUMBA anaswa na unga... Vigogo 10 kuhusika!!!




SAKATA la Morine Liyumba ambaye ni binti wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Utumishi  na Utawala wa Benki Kuu, Amatus Liyumba, kukamatwa na madawa ya kulevya ‘unga’, linawahusisha vigogo 10 Bongo.

Vyanzo visivyo na shaka vimetaja majina 10 ya vigogo ambao wanahusika katika mtandao ambao ndiyo uliokuwa unasafirisha madawa hayo ya kulevya kabla ya kukamatwa na Jeshi la Polisi Tanzania, Lindi.

Imedaiwa kuwa mtoto wa Liyumba na vijana wengine waliokamatwa ni ‘dagaa’ na kuongeza kwamba ‘papa’ wapo, siku wakitajwa taifa litatikisika kwa sababu majina yao ni makubwa na hadhi yao kijamii ipo juu.

“Hali ni mbaya, inasikitisha kwa sababu taifa linawaheshimu lakini wao ndiyo wahalifu. Wanaendesha mitandao hatari ya kuuza ‘unga’.  Vijana ambao ni nguvu kazi wanaharibika na kugeuka mateja kwa sababu yao,” kilisema chanzo chetu ambacho kinahifadhiwa jina.

Chanzo kingine kiliongeza: “Inatakiwa safari hii serikali iwe makini kwelikweli. Imeshaamua, kwa hiyo isisite kuchukua uamuzi mgumu. Hatutaki kuona majina ya watu yanaachwa kwenye hili sakata la kukamatwa kwa mtoto wa Liyumba. Wote wafikishwe mahakamani.”

Majina ya vigogo 10 ambao wanadaiwa kuwemo kwenye mtandao uliokuwa unasafirisha madawa ya kulevya kabla ya kukamatwa Lindi wiki iliyopita lakini yanahifadhiwa kwa sababu ya kukwepa kuvuruga upelelezi wa kipolisi.

Morine, alikamatwa pamoja na mfanyabiashara wa magari, Ismail Adamu au kwa jina lingine, Athuman Mohamed Nyaubi, 28, raia wa Tanzania anayeishi Afrika Kusini.

Mwingine aliyekamatwa ni dereva, Hemed Said, 27, mkazi wa Mtoni, Temeke, Dar es Salaam na Pendo Mohamed Cheusi, 67, mkazi wa Lindi ambaye ni mmiliki wa nyumba ambayo ilikutwa na madawa hayo.
Kwa upande mwingine, wananchi waliozungumza na Amani, wamemtaka Rais Jakaya Kikwete adumishe ulinzi kwa Kamanda wa Kikosi cha Kupambana na Kuzuia Madawa ya Kulevya Tanzania, Kamishna Mwandamizi Msaidizi wa Polisi, Godfrey Nzowa.

Wamesema kuwa Nzowa anapambana na watu wazito ambao wana fedha nyingi lakini kazi yake ina manufaa makubwa kwa nchi kutokana na kitendo cha idara yake kuwaokoa vijana na janga la matumizi ya madawa hayo.

Nzowa aliwahi kuliambia BLOG hii kuwa amekuwa akipokea simu mbalimbali za vitisho kutoka kwa watu asiowafahamu kutokana na kazi yake.

Alipoulizwa anafanya nini ili kujihami na watu hao, alisema mara nyingi huwa anamtegemea Mungu. “Mimi namtegemea sana Mungu na ndiyo maana mara zote utanikuta nikiwa na Kitabu cha Biblia Takatifu na huwa nasoma Zaburi ya 23.”

Comedy ZONE


There was a virgin who wanted to marry a farmer boy.

One day, she went to his parent's house for dinner. When they got done eating dinner, they decided to go for a walk through the pasture...

While they were walking, they came upon 2 horses that were mating. She looks at them with wonder because she has never seen anything like this before...

She asks the boy, 
"What are they doing?"

He says, 
"They're making love."

"Well, what's that long thing he's sticking in there?"

"Oh, uh, that's his rope," 
He answered.

"Well, what are those two round things on the other end?" She asked...

He says, "Those r his knots."

She says, 
"Oh, OK, I got it."

As they continue their stroll, they come to a man's house and go in....

She looks at him and says, 
"I want you to make love to me the way those animals were..."

Surprised and excited, the boy agrees...

While they are getting at it all hot and heavy, she grabs his balls and squeezes...

"Whoa, what are you doing?" He shouts!!!

The girl innocently replies, 
"I'm untying the knots so I'll get more rope!!! The rope z too short!!!"

Monday, January 23, 2012

Penzi la facebook lasababisha kifo cha mrembo...



Picha zinazosemekana kuwa ni za mrembo huyo baada kuuawa na mpenzi wake.

Mrembo aliyeuawa enzi za uhai wake.
UHUSIANO wa kimapenzi, ulioanzishwa kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook, umesababisha kifo cha mrembo nchini Nigeria.

Habari za mtandaoni zinadai kuwa mrembo huyo (jina halikutajwa) pamoja na boyfriend wake (jina pia halijatajwa), walikuwa kwenye uhusiano wa muda mrefu.

Imedaiwa kuwa wakati wawili hao wakiwa kwenye utekelezaji wa hatua za mwanzo za kufunga ndoa, mrembo huyo alimtaarifu boyfriend wake kuwa amepata mpenzi mwingine kwa njia ya Facebook.

Chanzo cha habari kiliiambia tovuti moja ya nchi hiyo kwamba mrembo huyo alianzisha urafiki wa Facebook na kijana mmoja raia wa Marekani (jina halijatajwa) kabla ya kibao kubadilika na kuwa wapenzi.

Chanzo kiliendelea kupasha habari kwamba mrembo huyo na mpenzi wake wa Facebook, walidumisha uhusiano wao kwa njia ya mawasiliano ya simu kwa muda mrefu kabla ya kukata shauri la kuonana ana kwa ana.

“Yule kijana raia wa Marekani alitembelea Nigeria, akafikia hoteli moja kubwa. Yule mrembo akaenda kukutana naye na kutumia muda mrefu chumbani.

“Ni kama baada ya kukutana ndiyo mapenzi yaliongezeka zaidi, kwani alipoondoka hotelini, yule mrembo alirudi kwa boyfriend wake aliyepanga kufunga naye ndoa na kumueleza kwamba mapenzi yamekwisha.

“Baada ya kuambiwa hivyo, kijana aliyekuwa na mategemeo ya kufunga ndoa na mrembo huyo, alimpeleleza mpenzi wake na kubaini mahali ambako kijana kutoka Marekani alifikia.

“Siku iliyofuata alivamia kwenye ile hoteli, akamkuta mpenzi wake na yule kijana wa Facebook, hapo ugomvi mkubwa ulizuka. Ugomvi haukuishia hapo kwa sababu kijana wa Nigeria aliahidi ni lazima aue mtu.

“Siku moja baada ya ugomvi hotelini, kijana wa Nigeria alimteka mpenzi wake na kumuua kwa kumkatakata na silaha inayodhaniwa kuwa ni panga,” alisema mtoa habari huyo.

Kwa mujibu wa mtandao huo mpaka pale habari hiyo inachapishwa, mtuhumiwa wa mauaji alikuwa hajakamatwa.

Mtoto wa NDIKU utata....





PAMOJA na nguvu kubwa inayotumiwa na wahusika kutuliza tuhuma ya staa wa ‘picha’ za Kibongo, Irene Uwoya ambaye ni mke wa Hamad Ndikumana ‘Kataut’ kuzaa na mwigizaji mwenzake, Kulwa Kikumba ‘Dude’, bado minong’ono mitaani inazidi kushika kasi mithili ya moto wa kifuu.


Uchunguzi umebaini kuwa baada ya skendo hiyo kuwekwa kweupe, watu walianza kufananisha picha kwa kulinganisha sura ya mtoto huyo aitwaye Krish na Dude wakipambanisha na Ndikumana.
“Kama kweli mtoto ni wa Hamad (Ndiku) na siyo Dude, kweli binadamu duniani ni wawiliwawili kwa namna mtoto huyo anavyofanana na Dude ukilinganisha na Hamad.



“Unajua picha inabeba meseji zaidi ya elfu moja hivyo kitendo cha watu kuanza kufananisha picha, ndicho kimeibua hayo yote. Hebu cheki mwenyewe, kweli ukianza kupambanisha picha, mtoto anafanana zaidi na Dude kuliko Ndiku, lakini kitaalamu siyo.



“Lakini kwa nini Dude? Mbona kuna watu wengi wako karibu na Irene na hawajahusishwa? Nadhani ili kumaliza utata, bora vipimo vya vinasaba (DNA) vichukuliwe ili tujue moja kuliko kila mtu kusema lake,” alisema mmoja wa mastaa wa filamu akiwa juu ya tuhuma hizo...



Ilielezwa kuwa tuhuma hiyo ndiyo chanzo cha kuyumba kwa ndoa ya Irene na mwanasoka huyo wa Kimataifa wa Rwanda.

MADAI YA SIKU NYINGI
Tangu mtoto huyo alipoanza kuonekana kwenye vyombo vya habari, siku chache baada ya kuona jua Mei, mwaka jana, kumekuwa na maneno ya tuhuma nzito kuwa siyo kopi ya jamaa huyo.

SIYO DUDE TU
Mbali na Dude kumekuwa na madai yakiwahusisha mastaa tofauti lakini zaidi ni kigogo mmoja serikalini ambaye pia ni mdau mkubwa wa burudani Bongo (jina tunalo).

UTETEZI WA DUDE
Mara kadhaa UTAMU ilimpa Dude nafasi ya kueleza kile anachokijua juu ya mtoto huyo ambapo alijitetea: “Hizi habari hata mimi nazishangaa, Irene ni msanii mwenzangu, ni rafiki yangu na hata mke wangu ni rafiki yake.



“Ukaribu wangu na Irene ulikuja wakati nafanya naye muvi, nahisi watu walituweka kwenye fungu la wapenzi kwa sababu hiyo ila ukweli ni kwamba siyo na sijawahi kuwa mpenzi wake.”
Baada ya kuona hali inazidi kuwa tete, hivi karibuni Dude alikuwa akimsaka Ndikumana ili kuzungumza naye juu ya suala hilo lakini alikana kueleza kiundani alichotaka kumwambia.
Hata hivyo, haikufahamika kama alifanikiwa kukutana naye.

UWOYA ANA SIRI MOYONI?
Mara zote Uwoya amekuwa akisisitiza kuwa mtoto ni wa Ndiku huku akibainisha kuwa siri ya baba wa mtoto huwa anakuwa nayo mama.



“Ni kweli anayejua baba wa mtoto ni mama. Ninachokijua mimi mtoto ni wa Hamad (Ndikumana).
“Hao wanaotajwa nafahamiana nao kama waigizaji wenzangu na marafiki tu, hakuna kitu kama hicho.
“Jamani! Ama kweli watu wana maneno, hivi huwa wanayatoa wapi? Kwa nini lakini? Hawajui hata sisi tunaumia? Hivi watu wanadhani mimi nina roho ya chuma? Hata mimi nina nyama kama wao, naomba waache kwani inaumiza kupita maelezo,” alisema.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...